Skip to main content

WAZIRI WA FEDHA AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI




Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango akihutubia wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa kujadili matumizi ya takwimu za umaskini na namna bora ya kupima hali ya umaskini Afrika jijini Dar es Salaam leo.


Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa akitoa hutuba yake.



Balozi wa Umoja wa Ulaya Kanda ya Afrika Mashariki, Roland Van De Geer, akitsoma hutuba yake.



Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird akizungumza kwenye mkutano huo.



Mtafiti kutoka Taasisi ya Repoa, Dk.Blandina Kilama, akizungumza kwenye mkutano huo.



Mtakwimu kutoka Menejimenti Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Tanzania Zanzibar, Mayasa Mwinyi akizungumza kwenye mkutano huo.



Taswira ya meza kuu.



Mkutano ukiendelea.





Taswira katika mkutano huo. 



Na Dotto Mwaibale

MATUMIZI ya Takwimu rasmi katika kupanga maendeleo ya wananchi kwa nchi zinazoendelea yamekuwa hayaendi kwa kasi inayotakiwa kimataifa imefahamika.






Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa Dar es Salaam leo wakati akisoma hutuba yake katika ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa kujadili matumizi ya takwimu za umaskini na namna bora ya kupima hali ya umaskini Afrika.

Alisema wakati dunia ikiendelea na utekelezaji wa malengo endelevu ya maendeleo ya dunia ya mwaka 2030 yapatayo 17, shabaha 169 na viashiria 231 ni dhahiri kuwa matumizi ya takwimu rasmi katika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake kila nchi haina budi kuyafanyia kazi ipasavyo.


"Kutokana na hali hiyo ndiyo maana Benki ya Dunia ikishirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango, Ofisi ya Taifa ya Takwimu imeona umuhimu wa kuwa na mkutano huu wa kimataifa wa kukutanisha watakwimu, wachumi na fani nyingine za kitaalam kujadili kwa kina matumizi ya takwimu za hali ya umaskini na tafsiri yake kwa ujumla na nini kifanyike ili kuboresha zaidi tafsiri ya umaskini" alisema Dk. Chuwa.

Katika hatua nyingine Dk.Chuwa alitoa angalizo kwa kuwaomba wadau wote wa ndani na nje ya nchi kuwa takwimu za hali ya umaskini pamoja na utafiti wa mapato na matumizi ya Kaya nchini zinatolewa na serikali hivyo zisitumike vibaya kuichafua nchi kuhusu hali ya umaskini.


Alisema iwapo itatokea kuwepo kwa matumizi mabaya sheria ya takwimu ya mwaka 2015 pamoja na kanuni zake tayari zimesainiwa zitachukua mkondo wake. 

Alisema Takwimu zitumike kwa lengo la kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi maskini wa Tanzania na kwa nchi zinazoendelea hususan kwa nchi zilizoko Kusini mwa Bara la Afrika.


Mgeni rasmi wa mkutano huo wa siku mbili ambao umeandaliwa na Benki ya Dunia, Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Philip Mpango alisema ilikuweza kujenga Afrika lenye neema nilazima kuhakikisha kuwa bara hili linaondokana na umaskini na kuwataka wataalamu waliohudhuria mkutano huo kutunganjia bora ya kupima umaskini.

Alisema ili kuendana na kasi ya dunia na utekelezaji wa malengo endelevu ya maendeleo ya mwaka 2030 yapatayo 17 ni wazi ufanyaji takwimu na utafiti unapaswa kufanyika ili kujua kiwango cha umaskini lakini pia aina ya umaskini uliopo.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...