Skip to main content

DC AVIPASHA VYOMBO VYA HABARI









IRINGA: Mkuu wa Wilaya ya Iringa (DC), Richard Kasesela avitaka vyombo vya habari nchini kutenga mafungu kwa ajili ya utafiti ukiwemo wa mafuta na gesi asilia.

Alisema kuwa masuala ya mafuta na gesi asilia yamepotoshwa kwa muda mrefu kutokana na wanahabari na vyombo vya habari kutowekeza katika utafiti, jambo ambalo linafanya wanahabri wengi kukwepa kuandika habari za utafiti au kupotosha jamii kwa lengo ya kuuza habari. 

DC Kasesela alitoa rai hiyo wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari ya namna ya kuandika masuala ya mafuta na gesi asilia yaliofanyika hivi karibuni mkoani Iringa.

Mafunzo hayo yalianaliwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikisha mikoa ya Njombe, Ruvuma na Iringa.

Alisema kuwa changamoto kubwa ya baadhi ya wanahabari huwa hawataki kujishughulisha na utafiti, kwani utafiti una gharama zake, jambo ambalo linafanya wanahabari wengi kukwepa kuandika habari za utafiti au kupotosha jamii ili mradi kuuza habari. 

“Vyombo vyetu vya habari havitoi fungu la utafiti jambo ambalo linafanya vyombo vingi vya habari aidha kukwepa kuandika habari hizi au kuandika kwa kupotosha jamii ili mradi auze habari,” alisema Kasesela.

Alisema kuwa ili kuhakikisha na kuimarisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia katika mkondo wa juu, kati na wa chini, vyombo vya habari havinabudi kutenga mafungu kwa ajili ya utafiti.

Alisema kuwa wanahabari nchini hawanabudi kuhabarisha jamii ili iweze kujua manufaa ya uwepo wa mafuta na gesi asilia ili wachangamkie fursa.

Mwaka 2015 Bunge la awamu ya nne ilipitisha sheria mpya kwa ajili ya kusimamia sekta ndogo ya mafuta nchini kwenye masuala ya utafitaji, uendelezaji, uzalishaji, usafirishaji, uingizaji, uchakataji, uhifadhi na biashara ya mafuta na gesi asilia nchini.

DC huyo alisema kuwa sheria hiyo ya mwaka 2015 imekuja kwa wakati muafaka ikiwa na nia njema ya kuhakikisha rasilimali hiyo inanufaisha taifa kwa ujumla.

Lengo likiwa ni kuhakikisha sekta ya mafuta nchini inakuwa endelevu na kulinda maslahi ya wadau wote kwa ustawi wa taifa na watanzania kwa ujumla.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...