Skip to main content

DHI NUREYN ISLAMIC FOUNDATION YATOA MSAADA VISIMA VYA MAJI KWA WANANCHI WA NDULI







Mmoja wa wananchi wa Kata ya Nduli katika Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa akijaribu kuvuta maji kutoka kwenye kisima cha maji. Kisima hicho ni mojawapo ya visima vinne vilivyotolewa msaada na taasisi ya Dhi Nureyn Islamic Foundation Iringa - Tanzania kwa kata hiyo hivi karibuni. (Picha Na Friday Simbaya)



Na Friday Simbaya, Iringa

Wananchi wa mitaa ya Kipululu na Igungandembwe, Kata ya Nduli katika Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa wameipongeza taasisi ya Dhi Nureyn Islamic Foundation Iringa - Tanzania kwa msaada wa visima vinne vya maji safi na salama hivi karibuni.

Wananchi hao kupitia Diwani wa Kata hiyo, Bashiri Mtove waliishukuru taasisi hiyo kwa kuwasaidia kupata visima vinne vya maji safi na salama na kuongeza kuwa miaka kwa zaidi ya 50 hawajawahi kupata maji safi na salama, ambapo hapo awali walikuwa wanatumia maji yasio safi na salama kutoka kwenye vikorongo vya maji.

Walisema kuwa kwa miaka mingi wamekuwa wakitumia maji yasio safi na salama kutokana na kutokuwepo kwa miundombinu ya maji ya bomba, lakini kupitia visima hivyo vya maji maisha yao yataboreka.

Maneno Mtove ni mkazi wa Mtaa wa Igungandembwe katika Kijiji cha Kigonzile alisema kuwa kwa miaka 50 hawajawahi kupata maji safi na salama isipokuwa walikuwa wanatumia maji ya korongoni ambayo si salama kwa afya.

“Tunashukuru sana taasisi ya Dhi Nureyn Islamic Foundation kwa kutusaidia kupata visima vya maji ambavyo vitasaidia kupunguza magonjwa ya homa za matumbo na pia wamejali afya zetu…” alisema Maneno Mtove. 

Kata ya Nduli ni mmoja ya kata zilizopo pembezoni mwa Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa ambazo hazina miundombinu za maji ya bomba ambapo wananchi wengi hutumia maji ya visima vifupi na kupelekea kuhatarisha maisha yao.

Kwa upande wake, msimamizi wa miradi ya Taasisi ya Dhi Nureyn Islamic Foundation Iringa-Tanzania, Faiz Said Abri alisema jana kuwa taasisi yake kwa kushirikiana na taasisi ile ya Al Muntada Aid ya Uingereza wameweza kuchimba visima vinne vyenye thamani ya shilingi 10,400,000/-, ambapo kisima kimoja kiligaharimu shilingi 2.6m/-.

Alisema kuwa taasisi yake kwa kushirikiana na Al Muntada Aid wameweza kuwachimbia visima vinne vya maji safi na salama wananchi wa mitaa ya Kipululu na Igungandembwe katika Kata ya Nduli, Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa.


Manispaa ya Iringa inaundwa na kata 18 na mitaa 192. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, kulikuwa na wakazi 151,345, wanaume wakiwa 71,932 na wanawake 79,413.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...