Skip to main content

MASHIRIKA YA UMMA JIANDAENI KUCHANGIA BAJETI YA SERIKALI




mkurugenzi miliki na miradi wa miradi wa kituo cha mikutano cha AICC Victoria Kamagenge akiwa anawaonyesha kamati Ya uwekezaji wa mitaji ya uma PAC moja ya mradi unaojegwa na kituo cha mikutano cha AICC jijini Arusha mradi unaogarimu kiasi cha shilingi bilioni 2.8












baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PAC) wakiwa wanateta jambo







wakiendelea kukagua



mbunge wa jimbo la Bunda mjini Ester Bulaya akiwa anakula na wakandarasi wa jengo jipya la maonyesho linalojengwa na kituo cha mikutano cha AICC wakati walipofanya ziara na Kamati ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PAC









Kamati ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PAC) wakiwa katika picha ya pamoja 



Na Woinde Shizza,,Arusha




Kamati ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PAC) imeyataka mashirika ya umma 265 yalilopo hapa nchini, kuanza kujiandaa kuchangia bajeti ya serikali kuanzia mwaka ujao wa fedha .




Aidha wakurugenzi na wenyeviti wa bodi wa mashirika hayo kuanzia mwakani watatakiwa kuwasilisha bajeti zao bungeni ili kuweza kupitishwa na bunge na hakuna shirika lolote la serikali litakaloweza kupiitishwa bajeti bila kuithinishwa na bunge.




Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo ,Albart Obama Mtabaliba mbunge wa jimbo la Buhigwe, mkoani Kigoma, wakati kamati hiyo ilipotembelea miradi ya kituo cha kimataifa cha mikutano (AICC)nakujionea miradi mbalimbali inayoendeshwa na kituo hicho ikiwemo ujenzi wa nyumba za kupangisha ,hosp italpamoja na jengo la maonyesho na mikutano linaloendelea kujengwa na kituo hicho.




Alisema kuwa licha ya mashirika hayo kuwa na thamani kubwa ya shilingi trilioni 26 lakini yamekuwa hayachangii ipasavyo bajeti ya serikali ,hivyo yanatakiwa yabadilike na kuanza kulipa kodi ipasavyo pamoja na kutoa gawio serikalini.




‘’Mashirika yote ya umma yaliyopo hapa nchini yanadhamani ya shilingi trilioni 26 na kwa mwaka yamekuwa yakitoa faida ya shilingi bilioni 450 pekee ,ambayo ni sawa na asilimia 1.08% kitu ambacho hakiwezekani ukilinganisha na mtaji uliopo wa trilioni 26 ,na hivyo wakurugenzi na wenyeviti wa bodi wametakiwa wahakikishe mapato yao kwa serikali yanapanda na angalau weweze kuchangia trilioni mbili kwa mwaka “alisema Mtabaliba




Akizunguzia kituo cha mikutano cha kimataifa AICC alipongeza miradi inayoendeshwa na kituo hicho na kushauri waanze kuchukuwa hatua ya kuanza kukabiliana na soko na pia wajitahidi kuwekeza zaidi katika ujenzi wa vituo vya mikutano vya kisasa ,na kuwataka kuelekeza nguvu zaidi ya kujenga kituo kikubwa cha mikutano katika mji mkuu wa Tanzania ambapo ni Dodoma.




Hata hivyo mmoja wa wabunge wa kamati hiyo,Ester Bulaya alikosoa gharama za ukarabati zilizotumika kukarabati ukumbi wa Simba hall uliopo katika kituo hicho ambapo kiasi cha shilingi bilioni tatu na nusu zilitumika jambo ambalo hawakuafiki na kushauri kwamba fedha hizo ninyingi sana na zingeweza kutumika kwenye uwekezaji mwingine .




Naye mkurugenzi mtendaji wa AICC Elishilia Kaaya alisema kuwa amefurahishwa na ujio wa kamati hiyo kuwatembelea na pia wamekutana nao na wamepewa elimu nzuri ya uwekezaji na wametaza baadhi ya mambo yale ambayo ayajaenda sawa wamewarekebisha pale ambapo awapo vyema wamewafundisha hivyo wanaamini walivyoambiwa mtazamo ubadili utabadilika kulingana na hali ilivyo.




Hata hivyo alisema kwa sasa wameanzisha mradi ujenzi wa kumbi za mikutano,mahoteli na maonyesho unaogarimu kiasi cha shilingi shilingi bilioni 2.8,mradi ambao unatarajiwa kukamilika mapema May 4 ambapo wanategemea utasaidia kuongeza mapato ya kituo hicho pamoja na ajira kwa watanzania.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...