Skip to main content

Pikniki Adui wa Mazingira Ukanda wa Utalii




Pikiniki zinazofanywa na watu mbalimbali katika fukwe zilizoko kwenye ukanda wa utalii visiwani Zanzibar, zinachangia uharibifu mkubwa wa mazingira unaotishia kuwakimbiza watalii.



Shughuli ya kusafisha mazingira iliyofanywa juzi katika eneo dogo kwenye ufukwe wa Muyuni ulioko Matemwe mkoa wa Kaskazini Unguja, ilikusanya karibu tani moja ya takataka zikiwemo chupa za plastiki.



Operesheni hiyo iliyochukua saa moja, ilijumuisha wafanyakazi wa Amber Resort na Best of Zanzibar, na kusafisha eneo linaoandaliwa kwa ajili ya mradi mkubwa wa kitalii utakaofanywa na kampuni ya Pennyroyal.



Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Meneja Mradi wa Amber Resort Murtaza Hassanali, alisema vijana wanaotembeza watalii (mapapasi) pamoja na wageni wanaofika hapo, huondoka wakiacha vitu vingi visivyofaa ambavyo hugeuka kuwa taka na sumu kwa viumbe wa baharini.



Aidha alieleza kuwa, pikiniki zinazofanywa na watu kutoka mjini na maeneo mengine hasa vijana, ni chanzo kikuu cha uharibifu wa fukwe hizo.



"Angalia ufukwe wote umejaa chupa za plastiki, karatasi za foili, mifuko na viatu visivyofaa na hakuna mtu anayejali kusafisha. Hii ni hatari sana kwa ustawi wa mazingira ya baharini," alisema.



Hata hivyo, alisema kampuni yake inakusudia kuubadilisha ufukwe huo kwa kusambaza vifaa vya kuwekea taka na kutoa elimu kwa wakaazi wa kijiji hicho juu ya umuhimu wa usafi wa mazingira.



Aidha alisema kwa kushirikiana na serikali ya wilaya kupitia ofisi ya halmashauri, wataandaa mabango ya matangazo yanayohimiza wananchi kuhifadhi fukwe na maeneo yote ya kijiji hicho na kuyaweka katika sehemu tafauti.



Kwa upande wake, Nahya Khamis Nassor, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) anayesomea elimu ya afya na mazingira, alisema inasikitisha kuona fukwe zinazotegemewa kuwa kivutio kwa watalii, zimekithiri uchafu bila uangalizi.



Alifahamisha kuwa, Kamisheni ya Utalii Zanzibar inafanya kazi kubwa ya kuvitangaza vivutio vilivyopo nchini kwa kusambaza vipeperushi vinavyoonesha uzuri wa mandhari pamoja na taarifa mbalimbali ili kuwashawishi watalii kuendelea kuja visiwani humu.



Hata hivyo, alisema pale watakapokuja na kukuta hali ni tafauti, watalii hao watahisi wamedanganywa na huenda wakafikiria mara mbili kabla hawajaamua kuja tena au hata kuvitangaza visiwa hivi kwa wananchi wenzao.



"Uchafu huu unaozagaa ufukweni unaishia baharini kwa kusombwa na maji yanapojaa. Plastiki haziozi na samaki wanaweza kuzila bila kukusudia na hii ni hatari kwa rasilimali za baharini kutoweka," alieleza Nahya.



Pamoja na kuwaomba wakaazi wa kijiji hicho kuzilinda na kuzihifadhi fukwe zao, aliishauri serikali ya wilaya kuunda kanuni maalumu zitakazosaidia kudhibiti uchafu unaotishia kuwakimbiza watalii.



Alisema itakuwa vyema, kanuni hizo ziweke adhabu ikiwemo faini kwa mtu yeyote atakaepatikana akichafua mazingira kwa makusudi kama inavyofanyika katika nchi na miji mingine.



Ofisa mratibu wa kampuni ya Amber Resort Mohammed Issa Khatib, alisema mpango huo utakuwa endelevu ili kuhakikisha elimu ya usafi wa mazingira inawafikia wananchi wote kijijini hapo na watu wengine wanaokitembelea ambao alisema ndio wanaoacha athari kubwa ya uchafu.



Aliwaomba wavuvi na vijana wanaofanya biashara za kitalii ufukweni waache kutupa taka ovyo, kwani kufanya hivyo kunachafua mandhari na taswira ya Zanzibar nzima mbele ya macho ya watalii.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...