Skip to main content

SHIRIKA LA EfG LAPUNGUZA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA SOKONI




Mwenyekiti wa Soko la Ilala Mchikichini, Jumanne Kongogo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu kupungua vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo baada ya kufanyika kampeni mbalimbali za kupinga ukatili huo zilizofanywa na Shirika la Equality for Growth (EfG) kwa kipindi cha miaka mitatu.






Mwenyekiti wa Soko la Kisutu, Taminu Chande, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu kupungua vitendo vya ukatili katika soko hilo. Kushoto ni Katibu wa soko hilo, Suitbert Nyawalla.



Mfanyabiashara wa soko la Ilala Mchikichini, Denis Ngaiza (kulia), akizungumza katika mkutano huo. Wengine ni wafanyabiashara wa soko hilo. Kutoka kushoto ni Yasin Kiluwa, Tatu Shehe na Samilla Kirundwa.



Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiashara katika Soko la Ilala Mchikichini, Betty Mtewele (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu kupungua kwa vitendo vya ukati wa kijinsia katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa elimu ya kupinga ukatili huo. Wengine ni wafanyabiashara wa soko hilo. 



Mwezeshaji wa kisheria katika soko la Ilala Mchikichini, Charles Beatus (katikati), akizungumza. Kulia ni Mwezeshaji wa kisheria, Eva Kakobe na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiashara katika Soko la Ilala Mchikichini, Betty Mtewele.



Mwezeshaji wa kisheria, Domitila Ngwada (kulia), akichangia jambo.



Mfanyabiashara wa Soko la Kisutu, Abdallah Mkumba (kulia), akichangia jambo. Kutoka kushoto ni Juma Khalid na Jumanne Ally.



Mfanyabiashara wa Soko la Kisutu, Rose Bruno, akizungumzia kupungua kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo.






Na Dotto Mwaibale


SHIRIKA la Equality for Growth (EfG) limetajwa kusaidia kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia katika masoko ya Ilala Mchikichini na Kisutu jijini Dar es Salaam.



Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara, viongozi wa masoko hayo pamoja na wasaidizi wa kisheria Dar es Salaam jana wamesema baada ya shirika hilo kutoa mafunzo na kufanya kampeni mbalimbali za kupinga ukatili huo hali imekuwa tofauti na awali.



"Soko letu la Mchikichini lilikuwa na kesi nyingi za vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kutokana na muingiliano wa watu hasa vijana kutoka katika maeneo yasiyo rasmi waliyokuwa wakifanyia biashara na kuhamia hapa kwetu" alisema Mwenyekiti wa soko hilo Jumanne Kongogo.



Alisema vijana wengi walihamia katika soko hilo wakitokea Manzese, Kariakoo, Mnazi Mmoja, Buguruni na maeneo mengine ya jiji na hata nje ya Mkoa wa Dar es Salaam.


Alisema baada ya EfG kufanya kampeni za kupinga ukatili huo na watuhumiwa kupigwa faini ya sh. 50,000 vitendo hivyo vimepungua kwa kiasi kikubwa.


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiashara katika soko hilo, Betty Mtewele alisema mafunzo waliyopata kupitia shirika hilo yamewafanya wanawake kujiamini na kushika nafasi mbalimbali za uongozi.


Mwezeshaji wa kisheria katika soko hilo Charles Beatus alisema matokeo ya kazi wanayoifanya ni makubwa mno baada ya kupata mafunzo kwa kuwezeshwa na shirika hilo.


Alisema kupitia kamati walioiunda wamefanikiwa kupunguza vitendo hivyo kwa asilimia kubwa kwani kupitia kamati hizo mtu akibainika kufanya udhalilishaji wowote amekuwa akiitwa mbele ya kamati.


Mwenyekiti wa Soko la Kisutu Tamimu Chande alisema katika soko hilo vitendo hivyo havipo na kama vitakuwepo basi vitakuwa vinafanyika kwa usiri bila wao kujua.


Katibu wa Soko hilo, Suitbert Nyawalle alisema mafunzo na kampeni zilizofanya na EfG katika soko hilo zimeonesha mafanikio makubwa.


"Niseme kuwa kampeni zilizofanywa na EfG zimewafanya wafanyabiashara katika soko hilo kujielewa na kujua kumfanyia mtu kitendo cha udhalilishaji pamoja na kumtukana ni kosa kisheria" alisema Nyawella.


Nyawella aliongeza kuwa mwaka juzi baada ya EfG kufanya tamasha la kupinga ukati wa kijinsia katika soko hilo kunamfanyabiashara mmoja alitenda kosa la udhalilishaji na alipopelekewa wito wa kuitwa alitoroka na mpaka leo hii hajarudi katika soko hilo kwa kuogopa asidakwe na mkono wa sheria.


Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa shirika hilo Shabani alisema shirika lao limekuwa likifanya kampeni ya kupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia katika Mkoa wa Dar es Salaam, Mwanza na Tanga na kwa Dar es Salaam wameendesha kampeni katika masoko ya Ilala Mchikichini, Temeke Sterio, Gezaulole, Ferry, Kisutu na Tabata Muslim.

Alisema kampeni yao ya kwanza ilikuwa ni Mpe Riziki na Si matusi na imesaidia sana wafanyabiashara kujielewa na kutambua suala zima la unyanyasaji wa kijinsia.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...