Skip to main content

ZAIDI YA 80 IRINGA WAPATA MAFUNZO YA UKARIMU NA UTALII


Mwenyekiti wa vikundi vya asili vya ngoma kutoka Ikwavila New Force katika Kijiji cha Mahuninga, tarafa ya Idodi wilayani Iringa, mkoani Iringa, Recktika Palinoo (wa mbele kulia) pamoja na katibu wake Leonatus Kikoti wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya ukarimu na utalii yaliyofanyika mkoani Iringa jana.  (Picha na Friday Simbaya)


MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka watoa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii kanda ya kusini kuboresha huduma zao ili kukidhi haja soko la utalii katika ukanda huu.

Alisema kuwa ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za taifa za kusini watoa huduma kwa kushirikiana na sekta binafsi hawanabudi kuinua viwango vya utowaji wa huduma.

Masenza alisema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watoa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii yaliyofanyika mkoani Iringa jana.

Alisema kuwa serikali ipo katika machakato wa kuboresha miundombinu za barabara na viwanja vya ndege ili kurahisha watalii kufika katika hifadhi pamoja na vivutio vilivyopo katka ukanda wa kusini.

Alisema kuwa takwimu za mwaka 2015 zinaonesha kuwa watalii wengi zaidi walitembelea mbuga za kanda za kaskazini kuliko kanda ya kusini, kwa hiyo mafunzo hayo yatakuwa chachu ya kuboresha utoaji wa huduma katika kanda ya kusini.

Zaidi wa washiriki wa 80 wamepata mafunzo ya ukarimu na utalii yaliaanza tarehe 22 hadi 24 Machi mwaka huu, yaliyotolewa na Chuo cha kitaifa cha utalii kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na SPANEST kwa ufadhili shirika la umoja wa mataifa la maendeleo (UNDP).

Alisema mafunzo hayo wamewaongezia ujuzi pamoja na kujiamini wakati wa kutoa huduma kwa watalii wanaotembelea ya kanda ya kusini.

Aidha, Masenza alisema Wizara ya Maliasili na Utalii ipo katika mchakato wa kutunga kanuni zitakazowazuia wafanyakazi wa hoteli wasio na vyeti vinavyotambulika na serikali kutoa huduma katika sekta ya utalii.

Alisema kuwa kanuni hiyo ambayo msingi wake unalenga kuendeleza na kuboresha huduma katika ya sekta hiyo, utahusisha pia kuvibana vyuo vya hoteli na utalii ili vitoe mafunzo yanayokidhi viwango.

“Baada ya kutungwa na kuanza kutumika kwa kanuni hizo, waajiri katika sekta hiyo watalazimika kuwaajiri wafanyakazi wenye sifa ambao wamesajiliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii,” alisema Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utalii, alisema Masenza.

Aliyasema hayo jana kwenye mafunzo ya siku tatu ya ukarimu na utalii yanayoshirikisha watoa huduma zaidi ya 80 wanaofanya biashara inayohudumia watalii mkoani Iringa.

Mafunzo hayo yanayotolewa na wizara hiyo kwa kushirikiana na Mradi wa Kuboresha Mtandao wa Maeneo Yaliyohifadhiwa Kusini mwa Tanzania (SPANEST), yanafanyika kwa siku tatu mjini Iringa.

Masenza alisema mafunzo hayo ya muda mfupi yameanza kutolewa katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini baada ya serikali kubaini baadhi ya vyuo vinavyotoa mafunzo hayo kuyatoa chini ya viwango.

Mratibu wa SPANEST, Godwell Ole Meing’ataki alisema changamoto hizo zimesababisha huduma duni katika maeneo ya mapokezi, chakula, vinywaji na malazi, na hivyo kuleta malalamiko makubwa sana kwa wageni.





Kwa kupitia mafunzo hayo mafupi Meing’ataki alisema; “ni mtarajio yetu maarifa watakayopata washiriki hawa yatawawezesha kutambua wajibu wao ili wageni wanaopata wapate huduma wanazotarajia.”

“Sekta ya utalii ina changamoto nyingi, lakini eneo hili la huduma ni muhimu kwasababu linaweza kusaidia kumrudisha mgeni tena na tena na kumfanya awe balozi kwa watu wengine,” alisema.

Kwa wawekezaji katika sekta hiyo, haitoshi tu kuwa na hoteli kubwa kama itakuwa haina huduma bora kwa wageni wake.

Awali, akifungua mafunzo hayo tarehe 22 Machi, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Fikira Kissimba alisema licha ya ukanda wa nyanda za juu kusini kuwa na vivutio vingi vya utalii, idadi ya watalii wanaovitembelea ni ndogo na moja ya sababu yake ni uduni wa huduma katika sekta hiyo ya utalii.


Akishukuru wizara ya maliasili na utalii na SPANEST kwa kutoa mafunzo hayo, Kissimba alisema yatakuwa chachu katika kukuza na kuendeleza utalii kusini mwa Tanzania kwa kutoa huduma bora kwa watalii.

Aliwataka wahudumu katika sekta hiyo waache tabia ya uvivu, kufanyakazi kwa mazoea na wawe wepesi kujifunza ili kuboresha huduma zao.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...