Skip to main content

DC KASESELA APIGA MARUFUKU UVUAJI SAMAKI WACHANGA BWAWA LA MTERA

Na Friday Simbaya, Iringa, zana haramu za uvuvi za chomwa moto Migoli





IRINGA: Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela amepiga marufuku uvuaji wa samaki wachanga walio chini ya kiwango kinachoruhusiwa cha inchi tatu (3) kuankochangia uharibifu wa mazalia ya samaki katika Bwawa la Mtera. 

Alisema kuwa kwa muda mrefu Bwawa la Mtera limekuwa likikabiliwa na tatizo la uvuvi haramu unaotumia zana haramu za uvuvi kama vile nyavu za kokoro, gonga, kimia na katuli. 

Kasesela alitoa agizo hilo jana wakati wa zoezi la uteketezaji wa zana haramu za uvuvi 124 kwa moto lililofanyika katika Kijiji cha Migoli, Taarafa ya Isimani wilayani Iringa, mkoani Iringa. 

Alisema kuwa uvuvi haramu umepelekea kupunguza kiwango cha samaki katika Bwawa la Mtera kwa kuvua samaki wachanga walio chini ya inchi tatu (3) na kupelekea uharibifu wa mazalia ya samaki. 

“Uwepo wa bwawa hili umekuwa na faida kwa jamii, umewezesha shughuli za uvuvi kuwaongezea kipato na kuboresha lishe katika jamii kwa vile karibu asilimia 90 ya wananchi wa vijiji vinavyoishi karibu na bwawa hilo vinalitegemea,’ alisema Kasesela. 

Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ina eneo la kilometa 220 za bwawa hilo ambapo linajumuisha Kata ya Migoli katika vijiji vya Kinyali, Mbweleli, Makatapola, Mtera, Mtera, Migoli na Mapera na Kata ya Izazi katika vijiji vya Mnadani na Makuka. 

Naye, Diwani wa Kata ya Migoli, Majaliwa Lyaki (CHADEMA) alisema kuwa zoezi la kupiga marufuku uvuvi haramu katika Bwawa la Mtera halitakuwa na tija kama upande wa pili la bwawa hilo wanaendelea kuvua samaki kwa kutumia zana haramu za uvuvi. 

Alisema kuwa Bwawa la Mtera lipo katika eneo linalozinguka Halmashauri za Chamwino na Mpwapwa katika mkoa wa Dodoma na Halmashauri ya Iringa katika mkoa wa Iringa. 

“Ili kuwepo na uvuvi endelevu katika Bwawa la Mtera uvuvi haramu katika upande wa halmashauri za chimwino na Mpwapwa Mkoa wa Dodoma lazima udhhibitiwe…, ” alisema Lyaki. 

Kwa upande wake, Ofisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mathew Sanga alisema kuwa katika kudhibiti uvuvi haramu wamefanyikwa kukamata zana haramu 124 na samaki wachanga kilo 7,227 na watuhumiwa 16 walikamatwa. 

Alisema kuwa watuhumiwa hao walipelekwa mahakamani ambapo kati yao 12 walikutwa na makosa na nne (4) kesi zao bado zinaendelea mahakamani. 

Sanga alibaini kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa inakabiliwa na uvuvi haramu na hili kukomesha vitendo hivyo wamekuwa wakifanya doria na kutoa elimu kwa wavuvi, wafanyabiashara na wasafirishaji wa samaki. 

Aidha Halmashauri iliitisha mkutano tarehe 29.03.2017 ambapo wavuvi na wasafirishaji 121 walishiriki, lengo likiwa ni kutoa elimu kwa wasafirishaji wa samaki, wanunuzi wa samaki na wavuvi kuzingatia sheria namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009. 

Kanuni hizo zinamtaka kila mmoja kufanya biashara akiwa na leseni ya uvuvi na biashara ya samaki pamoja na matumizi ya nyavu zenye inchi tatu ili kutovua samaki wachanga. 

Bwawa la Mtera lina ukubwa wa kilometa za mraba 660 na linalozunguka Halmashauri za Chamwino na Mpwapwa katika Mkoa wa Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika Mkoa wa Iringa.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...