Skip to main content

IHEMI WATAKIWA KUFANYA ULINZI SHIRIKISHI VYANZO VYA MAJI

IRINGA: Serikali ya Kijiji cha Ihemi imetakiwa kufanya ulinzi shirikishi kulinda chanzo cha maji cha Ihemi ili kiendelee kutiririsha maji muda wote.

Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa kikosi kazi namba tatu cha kunusuru ikolojia ya bonde la mto Ruaha mkuu ili liweze kurudi katika hali yake ya kawaida ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu jana katika kijiji cha Ihemi kilichopo katika kata ya Ifunda wilayani Iringa.

Ayubu alisema “serikali ya kijiji cha Ihemi inawajibu wa kulinda chanzo cha maji hiki cha Ihemi. Tena ulinzi huu lazima uwe shirikishi ukihusisha wanufaika wote, hasa wakulima na wafugaji”. Aliongeza kuwa mifugo imekuwa ikilishwa katika chanzo hicho cha maji na kupiga marufuku utaratibu huo wa kulisha mifugo katika chanzo hicho. Aidha, aliitaka Halmashauri ya wilaya ya Iringa kutoa ushauri wa kitaalamu katika kutatua changamoto za kiuhifadhi kwa vijiji vyote vinavyozunguka vyanzo vya maji wilayani humo. “Halmashauri ya wilaya ya Iringa nyie ndiyo wasimamizi wa hivi vijiji, pia mnao wataalamu wa kutosha, hivyo, hakikisheni mnavitembelea vyanzo hivyo vya maji na kushauri kitaalamu juu ya uhifadhi wake ili viwe endelevu” alisisitiza Ayubu.

Awali Diwani wa Kata ya Ifunda, Elikus Ngweta alikiomba kikosi kazi hicho kuangalia uwezekano wa kuijengea uwezo jumuiya ya watumia maji bonde dogo la mto Lyandembela ili iweze kutekeleza majukumu yake vizuri. Vilevile, aliahidi kuendelea kusimamia utunzaji wa vyanzo vya maji katika Kata ya ifunda. “Mheshimiwa mwenyekiti wa kikosi kazi hiki, tunaahidi kutokana na umuhimu wa maji na kuwa maji ni uhai, na bila maji hakuna maisha, sisi tutasimamia utunzaji wa vyanzo vya maji ili viwe endelevu” alisisitiza Ngweta.

Kikosi kazi cha kurudisha ikolojia ya bonde la mto Ruaha mkuu kiliundwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...