Skip to main content

MADEREVA 20 KUSHIRIKI MASINDANO YA MAGARI MKOANI IRINGA


Mshiriki wa mashindano ya mbio za magari kutoka Iringa (Mkwawa Rally Team), Ahmed Huwel ambaye atatumia gari lake mpya aina ya Ford Fiesta akimkaribisha Dereva mkongwe wa mbio za magari nchini Gerald Miller (wa pili kulia) kutoka mkoani Arusha alipowasili jana, kwa ajili ya kushiriki mashindano ya mbio za magari yatakayofanyika kuanzia tarehe 22-23, mwezi Aprili mwaka huu mkoani Iringa. Mashindano hayo yanayoandaliwa na klabu ya mbio za magari ya Iringa (IMSC) kwa kushirikiana na kiwanda cha maji cha Mkwawa cha mjini Iringa. (Picha na Friday Simbaya)


Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wanahabari jana kuhusu Mashindano ya mbio za magari kitaifa yatakayoshirikisha madereva 20 wakiwa pamoja na wasaidizi wao kutoka ndani na nje ya nchi yanayoandaliwa na klabu ya mbio za magari ya Iringa (IMSC) kwa kushirikiana na kiwanda cha maji cha Mkwawa cha mjini Iringa. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa IMSC Hamid Mbatta na kushoto kwake ni Afande Steven Nyandongo wa kikosi cha usalama barabarani -Iringa na Mwasisi wa mashindano hayo mkoani Iringa Francis Mwakatundu.(Picha na Friday Simbaya)

Dereva mkongwe wa mbio za magari nchini Gerald Miller kutoka mkoani Arusha akikagua gari lake aina ya Mitsubishi baada ya kuwasili mjini Iringa jana kwa ajili ya kushiriki mashindano ya mbio za magari yatakayofanyika kuanzia tarehe 22-23, mwezi Aprili mwaka huu mkoani Iringa. Mashindano hayo kitaifa yatashirikisha madereva 20 wakiwa pamoja na wasaidizi wao kutoka ndani na nje ya nchi yanayoandaliwa na klabu ya mbio za magari ya Iringa (IMSC) kwa kushirikiana na kiwanda cha maji cha Mkwawa cha mjini Iringa. (Picha na Friday Simbaya)


Mwenyekiti wa chama cha mbio za magari mkoa wa Iringa (IMSC) Hamid Mbatta amewataka wananchi mkoani iringa kutumia fursa ya mashindano ya mbio za magari kukuza biashara kutokana na wageni wengi watakaofika mkoani hapa kushuhudia mashindano hayo.

Alisema kuwa zaidi ya wageni 500 na madereva 20 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajia kushuhudia na kushiriki mashindano ya mbio za magari kitaifa yatakayofanyika mkoani iringa kuanzia tarehe 22-23, Aprili mwaka huu.

Mbatta alisema kuwa mashindano ya magari ni fursa kubwa kwa kufanya biashara pamoja na kukuza na kuimarisha sekta ya utalii kanda ya kusini.

Alisema kuwa kuna njia tano zilizochaguliwa kwa ajili ya mashindano ambapo zaidi ya Km 302 (completion section na transport section) kuanzia kiwanda cha maji cha mkwawa kilichopo mjini iringa ambao ni wadhamini wakubwa wa mashindano hao.

Alitaja washiriki kutoka mkoani Iringa (Mkwawa Rally Team) kuwa ni ahmed Huwel akiwa na msaidizi wake Maisam Fazal ambaye alitumia gari lake mpya aina ya Ford Fiesta na Hamid Mbatta akiwa na msaidizi wake (navigator) sultan Chana.

Mwingine aliyeomba aliomba kushiriki kupitia Mkwawa Rally Team ni Shanto ambaye atakuwa na msaidizi wake Rahim.

Mwenyekiti wa chama cha mbio za magari mkoa wa Iringa Hamid Mbatta alisema kuwa mkoa wa Iringa hadi sasa umeendelea kufanya vema kwenye mashindano hayo na upo uwezekano mkubwa wa kushiriki mashindano ya kimataifa.

Mwasisi wa mashindano hayo Francis Mwakatundu alisema kuwa Iringa ni tishio kwa mashindano hayo.

Pia dereva mkongwe wa mbio za magari nchini Gerald Miller kutoka mkoani Arusha na davis Mosha wamethibitisha kushiriki mashandano hayo.

Kwa upande wake, mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza Amewataka wananchi wa mkoa wa Iringa kuchukua tahadhari wakati wa mashindano ya mbio za magari.

Akizungumza jana na wanahabari Kasesela alisema kwa siku ya Jumamosi na jumapili wakati mashindano hayo ya mbio za magari zilizodhaminiwa na kiwanda cha maji Mkwawa kuwa ni sehemu ya ukuaji wa uchumi wa mkoa.

Alisema kuwa kupitia mashindano hayo upo uwezekano mkubwa wa mkoa wa Iringa kuingia katika mashindano ya kimataifa ya mbio za magari.

Pia alisema kupitia mashindano hayo upo uwezekano mkubwa wa kutangaza hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Aidha alisema kuwa kwa wazazi wanapaswa kuwa makini na watoto pamoja na waendesha bodaboda kuacha kufukuza magari ya mashindano.

Naye Afande Steven Nyandongo wa kikosi cha usalama barabarani -Iringa amekitaka chama cha mbio za magari mkoa wa Iringa pamoja na washiriki wa mashindano hayo kuhakikisha wanaweka usalama kwanza ikiwa pamoja na kufuata sheria za usalama barabarani. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...