Skip to main content

MAKOTA FOREST YAKABIDHI BATI 20 NA MIFUKO YA CEMENT 100 KWA MKUU WA WILAYA KILOLO



Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah (kushoto) akipokea msaada wa madawati 20 kutoka kwa mkurugenzi wa kampuni ya Makota Forest Bharat Bhesania jana kampuni hiyo imetoa madawati hayo pamoja na bati 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu.





KAMPUNI ya Makota Forest ya inayojihusisha na shughuli za Kilimo katika kata ya Ihimbo wilaya ya Kilolo mkoani Iringa imetoa msaada wa bati 100 pamoja na madawati 20 kwa ajili ya kuunga mkono serikali ya wilaya ya Kilolo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa .


Akizungumza leo [jana] wakati wa kukabidhi msaada huo kwa mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah ,Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bharat Bhesania alisema kuwa kampuni yake itaendelea kusaidia shughuli mbali mbali za kimaendeleo katika wilaya ya Kilolo na maeneo mengine ya mkoa wa Iringa .


Bhesania alisema kuwa jitihada zinazofanywa na viongozi wa wilaya ya Kilolo na mkoa wa Iringa katika kuwaletea wananchi maendeleo ni jitihada ambazo zinapaswa kuungwa mkono na wadau wote wa maendeleo ndani ya mkoa huo na waliopo nje ya mkoa .


" Sisi kama wawekezaji tunaowajibu wa kuunga mkono shughuli zote za kimaendeleo zinazoendelea katika maeneo yetu ....nimekuwa nikisaidia shughuli nyingi sana na sichoki kuendelea kusaidia "Alisema Bhesania


Kwa pande wake Meneja wa kampuni Gibson Mkuvalwa alisema kampuni yake inajihusisha na kilimo cha mahindi na mwaka huu ndipo shamba hili limeanza ila changamoto kubwa wanayokutana nayo ni kodi kubwa wanayolipa na kuomba serikali kuweza kuliangalia hilo.


Mkuvalwa alisema kupitia kampuni hiyo wameweza kutoa ajira kwa wananchi wanaozunguka kampuni hiyo na wamekuwa wakijitolea kutengeneza barabara na kushiriki kwa nguvu zote kuunga mkono shughuli za kimaendeleo .


Nae Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia alisema kuwa kuwa mwekezaji huyo ameanza kufungua rasmi mlango wa wawekezaji na wadau wa maenbdeleo Kilolo kuanza kuchangia bati na madawati na kuwa amepata kufanya ziara ndani ya wilaya hiyo na nje ya wilaya kwenda kuwaomba wawekezaji na wadau wa maendeleo waliopo nje ya Kilolo kusaidia harambee hiyo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu .


Alisema kuwa msaada huo wa kampuni ya Makota Forest ni mwanzo wa wadau wengine kujitokeza kusaidia harambee hiyo na kuwaomba wawekezaji wengine kujitokeza .


Hezron Nganyagwa ni Diwani wa kata ya Ihimbowilayani humo nae aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo alisema kuwa utasaidia kwa matumizi ya shule iliyokumbwa na maafa ya kuezuliwa ambayo wananchi wameanza ujenzi wa kuta .

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...