Skip to main content

POLISI DAR YAWATIA MBARONI WATU 267



Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata watuhumiwa 267 kwa makosa mbalimbali ikiwemo unyang’anyi wa kutumia silaha, utapeli, wizi, kucheza kamari, na kupatikana kwa dawa za kulevya, kuanzia Aprili 13 hadi 17,2017.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 19, 2017 Jijini Dar es Salaam, Kamishna wa kanda hiyo, Kamanda Simon Sirro amesema takribani kete 366 za dawa za kulevya, bhangi misokoto 51 na lita 200 za pombe haramu aina ya gongo zilikamatwa kufuatia operesheni kali iliyofanywa na askari polisi.

“Pia Polisi wamekamata watuhumiwa watatu kwa wizi wa vitu mbalimbali maeneo ya Chamanzi wanaofahamika kwa majina ya Athuman Bashiru na Rashid Seleman na Mohamed Mussa. Pia wamekamata pikipiki moja ya wizi na kwamba watuhumiwa wawili wanashikiliwa kufuatia tukio hilo ambapo walimkata na panga kichwani mmiliki wake Ibrahim Shaban na kumpora pikipiki hiyo,” amesema.

Aidha, amesema Jeshi la Polisi mnamo Aprili 10, 2017 limekamata watuhumiwa watano wa ujambazi ambao hushirikiana kufanya matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali ya jiji.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Salimu Matanda, Eliaki Chaki, Shaban, Rashid Said, na Nassoro Choro ambao wamekamatwa baada ya kuiba pikipiki aina ya Boxer inayomilikiwa na Noel Mkinga.

Katika tukio lingine, Kamanda Sirro amesema Jeshi la Polisi lilikamata silaha moja aina ya Shotgun maeneo ya Kiwalani iliyofutwa namba za usajiri baada ya wahalifu waliokuwa nayo kuitekeleza walipokuwa wanakimbizwa na Polisi

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...