Skip to main content

VIJANA WASHAURIWA KUUNGA MKONO MABADILIKO NDANI YA CHAMA


Wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo mkoani Iringa ambao ni wanachama cha CCM wakiitikia salama kutoka kwa katibu wa masuala ya kisiasa na mahusiano ya kimataifa Kanal mstaafu Ngemela Lubinga  kwenye mkutano wa CCM  uliyofanyika mjini Iringa juzi. (Picha na Friday Simbaya)







Katibu wa masuala ya kisiasa na mahusiano ya kimataifa Kanal mstaafu Ngemela Lubinga akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo mkoani Iringa juzi. (Picha na Friday Simbaya)



CHAMA Cha mapinduzi (CCM )kimewataka vijana kuunga mkono mabadiliko yanayofanywa na chama hicho ka kuwa yanalnga kuleta ufanisi ya chama. 

Kauli hiyo na katibu wa masuala ya kisiasa na mahusiano ya kimataifa Kanal mstaafu Ngemela Lubinga juzi kwenye mkutano wa CCM wakati akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo mkoani Iringa ambao ni wanachama cha CCM. 

Alisema kuwa kuna watu wanabeza mabadiliko yaliyofanywa na chama hicho hivi karibuni mjini Dodoma na kuongeza kuwa mabadiliko hayo yanalenga kuboresha utendaji ndani ya chama. 

Viongozi wa CCM wa kata na matawi pamoja na wananchi mbalimbali waliohudhuria mkutano huo uliyofanyika mjini Iringa juzi. 

Lubinga alisema kuwa viongozi walioteuliwa na rais ambao wameondolewa kwenye nyadhifa mbalimbali kuacha kupiga kelele na hivyo kutaka walioondolewa kuyakubali mabadiliko ya mfumo, huku akiwataka walioondolewa kuheshimu busara za Ikulu kwa maamuzi hayo. 

“Rais anapoteuwa viongozi wake kuwapa dhamana anaona kwamba wewe anakuhitaji katika nafasi hiyo na mazingira yaliyopo yanakuhitaji unaweza kuyamudu, lakini inapofika wakati anakuondoa ujue kwamba mazingira yale huwezi kuyamudu na anakuokoa ili usipate laana.”alisema Lubinga. 

Alisema kuwa busara za Ikulu ziheshimewe na zisijadiliwe kwamba na hasitoke mtu akasma sijapata kwa sababu baadhi ya viongozi wameondolewa madarakani lakini wamebaki wakilalamika mitaani hovyo. 

Lubinga alisema chama hicho kimejipanga kimkakati kuhakikisha kinajenga nidhamu na uwajibikaji ndani ya serikali na kuwaondoa watendaji wote ambao wanaonekana kuwa kikwazo katika utekelezaji wa mipango ya serikali ya kujenga uchumi imara kupitia sekta ya viwanda na uzalishaji. 


Alisema kuwa chama wakati kinafanya mabadiliko kilichukua hatua ya kuona wapi kinakwama na nani anakikwamisha kwa kula rushwa au kwa kuwa mnafiki. 


Kanali Lubinga alisema kuwa hatua iliyochukuliwa kwa kuona kwamba kinafanya kitu chenye uhakika kikaona kwamba watu waovu waondolewe ndani ya chama. 


“Maoni yalikuja kila mtu aliitwa na kujieleza na alipojieleza alitolewa ushahidi wa kutosha kwamba wewe… unakubali au unakataa na ndio hao wameondolewa kwa kuona walikisaliti chama.”alisema Lubinga. 


Katika hatua nyingine alisema kuwa waliosababisha jimbo la Iringa mjini kupotea sio wananchi wapiga kura bali ni viongozi wake. 


“Iringa mmeona viongozi wa juu walitupa matatizo, Iringa bado kuna shida kidogo, kuna vita vya ndani kwa ndani, bado kuna maadui wadogowadogo na mkiamua mtayamaliza, lakini kiukweli waliosababisha kupoteza jimbo la Iringa kupotea sio wananchi wapiga kura waliwapa kura vizuri kabisa bali ni viongozi wake ndio waliofanya mkalipoteza sasa jengeni Iringa Mpya. 


Alisema kuwa kusudio la CCM kufanya mabadiliko ya kuwaondoa watu waovu ni kusudio zuri na wale ambao kama wapo wengine wajiandae. 

“Tunalalamika rushwa mmeona madhara ya rushwa katika shughuli zenu za kila siku na ninyi wananchi mmeona matatizo yenu ambayo yanatokana na rushwa sasa hao watu wa nini ndani ya chama?alihoji Lubinga. 


Pia alisema kuwa chama kimemua kufanya mabadiliko ili kuendana na hitaji,jamii yoyote duniani inayo utaratibu wake wa kutimiza wajibu wake ili iweze kuendana na hitaji liliopo mabadiliko katika uongozi na mabadiliko katika utendaji. 

Aidha aliongeza kuwa CCM katika kujifanyia kujitathimini chenyewe kimeamua kupunguza idadi ya vikao ndani ya chama, kupunguza idadi ya wajumbe kwa baadhi ya vikao na kurudisha madaraka chini kwa wananchi ili mambo yaende vizuri. 

Kwa upande wao katibu wa (UVCCM) Mkoa wa Iringa Abdulikarim Halanga na Marko Mbanga ambaye ni katibu wa CCM wilaya ya Iringa waliwataka wana CCM hao kuwa waadilifu na wazalendo kwa sababu mbadiliko hayo ni ya kukijenga chama kuwa CCM mpya na Tanzania mpya.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...