Skip to main content

Wagombea wa Chadema Washindwa Ubunge wa Afrika Mashariki…!!!

Lawrence Masha na Friday Simbaya leo Dodoma (Picha na Chris Jr Simbaya)


Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamewachagua wajumbe 7 wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania huku wagombea wawili wa CHADEMA wakipigiwa kura za ‘HAPANA’ na hivyo kushindwa kupitishwa.

Wagombea hao wa CHADEMA ni Lawrence Masha na Ezekiel Wenje, ambao pia waliungana na wagombea wengine wote kujieleza mbele ya wabunge kabla ya zoezi la upigaji kura.
Kwa upande wa CCM, walioshinda ni

1. Fancy Nkuhi
2. Happiness Legiko
3. Maryam Ussi Yahya
4. Dkt Abdullah Makame
5. Dkt Ngwaru Maghembe
6. Alhaj Adam Kimbisa

CUF iliyokuwa na wagombea watatu kwa ajili ya nafasi moja, aliyeshinda ni Mohamed Habib Mnyaa akiwashinda Twaha Taslima na Sonia Magogo

Awali palitokea mabishano ya kikanuni juu ya wagombea wa CHADEMA yaliyosabaishwa na chama hicho kuweka wagombea wawili pekee wakati nafasi kwa ajili ya chama hicho zikiwa mbili pia.

Baadhi ya wabunge walitaka Spika atumie utaratibu wa kuwahoji wabunge kama wnawakubali ama lah, huku wabunge wa CHADEMA wakitaka wagombea hao wapigiwe kura sawa na wengine, ambapo wapiga kura wangelazimika kupiga kura za kuwakubali wagombea hao hata kama hawawataki.

Baada ya mvutano wa takriban saa moja, Spika Job Ndugai aliamua kura zipigwe, lakini kwa kundi la wagombea wa CHADEMA akaelekeza kuwa wapiga kura wa uhuru wa kuweka alama ya ‘tick’ kama wanamkubali mgombea au alama ya ‘X’ kama hawamkubali.

“Sasa maelekezo yangu ni kwamba ukifika kwa wagombea wa Chadema weka X kama humtaki, na weka tick kama unamtaka” Alihitimisha Ndugai

Akizungumza baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo majira ya saa 7 usiku, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe amesema haki haikutendeka ikiwa ni pamoja na ubabe kutumika na upindishwaji wa kanuni, hivyo watakwenda kuitafuta haki yao mahakamani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...