Skip to main content

MKOA WA IRINGA UNA UPUNGUFU WA WALIMU 1,581


 
Afisa ya Elimu wa Mkoa wa Iringa Richard Mfugale (Picha na Maktaba)



Mkoa wa Iringa una upungufu wa walimu 1,581 katika shule za msingi na sekondari kwa shule za Serikali, imefahamika. 


Katika shule za msingi upungufu ni walimu 984 na shule za sekondari ni upungufu wa walimu 597 katika masomo ya sayansi. 


Hayo yalielezwa hivi karibuni na Afisa Elimu Mkoa wa Iringa, Richard Mfugale wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kwa mwaka 2017, yanakusudia kutumika kutoa msukumo mpya katika kuendeleza elimu hasa uimarishaji wa umahiri wa misingi ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK). 


Aidha afisa elimu huyo alisema kuwa Idadi ya walimu katika Shule za Sekondari za Serikali Mkoa ni jumla ya walimu 3,390 kati ya hao Walimu 837 ni walimu wa sayansi na walimu 2,553 ni wa masomo ya sanaa. 


Wakati idadi ya walimu katika Shule za Msingi za Serikali, mkoa unahitaji kuwa na walimu 6,240, waliopo ni walimu 5,256 na upungufu ni walimu 984. 


Mfugale pia alisema ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari, jumla ya vyumba vya maabara 321 vinahitajika. 


Kwa upande wa nyumba za walimu shule za serikali alisema zilizopo ni 559 mahitaji ni nyumba 2,880 na matundu ya vyoo yaliyopo ni 2,174 ikilinganishwa na mahitaji ya matundu 2679. 


Mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya kusoma kwa Mkoa wa IRINGA alikuwa Mkuu wa Wilaya wa Mufindi, Jamhuri William kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza ambayo yalianza tarehe 19/05/2017 na kuihitimishwa kimkoa tarehe 25/05/2017 katika Halmashauri ya Mji wa MAFINGA ambapo Halmashauri zote za Mkoa wa Iringa zilishiriki kikamilifu baada ya kuwa zimefanya maadhimisho hayo katika ngazi ya Halmashauri. 



Alisema Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kwa mwaka 2017 yalikusudia kutumika kutoa msukumo mpya katika kuendeleza elimu, hasa uimarishaji wa umahiri wa misingi ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK). 


Masenza alisema kuwa serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Rais Dr. John Pombe Magufuli inafanya juhudi za dhati za kuhakikisha kuwa elimu inaboreshwa na kuondoa baadhi ya michango isiyo ya lazima kwa utekelezaji wa Elimu bila Malipo. 


Kaulimbiu mwaka huu inasema: “Ufundishaji bora wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu ni msingi wa maarifa, ujuzi na maendeleo ya elimu katika kufikia uchumi wa viwanda”. 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...