Skip to main content

UHAMBILA ACHENI KUHARIBU VYANZO VYA MAJI NA MALIASILI ZENU


viongozi wa shirika la LEAT pamoja na viongozi wa kijiji cha Uhambila wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wakati wa kujadili maswala ya utunzaji wa Maliasili na vyanzo vya maji vilivyopo eneo hill.
Baadhi ya wananchi wakisikiliza kinachoendelea kwenye mkutano wa kijiji wa kujadili maswala ya utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja Maliasili za kijiji hicho.


Na Fredy Mgunda, Iringa.

Wananchi wa kijiji cha uhambila wilayani Mufindi Mkoani Iringa wametakiwa kutunza na kuvilinda vyanzo vya maji na maliasili zilizopo katika kijiji hicho.


Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara wa kijiji hicho Afisa mradi kutoka shirika la LEAT upande wa wilaya ya mufindi Jamali Juma alisema kuwa wananchi wanatakiwa kujiepusha na ukataji miti hovyo na kulima vinyungu kwenye vyanzo vya maji kwa kuwa kufanya hivyo kunasababisha ukame.


"Mkiangalia zamani maeneo haya yalikuwa ya kijani na tulikuwa na mito midogo midogo mingi iliyokuwa inatililisha maji msimu mzima lakini hali ya sasa haipo hivyo kutokana na kutaka miti na kuaharibu vyanzo maji nawaomba wananchi acheni hiyo tabia ili tuwe na Mazingira mazuri kama zamani"alisema juma


Ukataji miti na uharibifu wa vyanzo unasababisha madhara mengi makubwa na ndio maana tunaona sasa kumekuwa na magonjwa mengi ambayo yanaathari ya moja kwa moja kwa mwanadamu lakini pia uharibifu huo husababisha mabadiliko ya vipindi vya mvua na kukosekana kwa mvua za kutosha.


Juma alisema kuwa dunia kwa sasa inakabiliana na swala la mabadiliko ya tabia nchi hata hivyo wananchi mnatakiwa kuwa umakini ili msije mkaishi kwenye jangwa kutokana na uharibifu wetu.


"Ni kosa la jinai kwa mtu yoyote yule kukata miti bila kibali au kuharibu vyanzo vya maji kutokana na sheria zetu za mwaka 1982 hivyo kukata miti au kuaribu vyanzo vya maji sio haki ya msingi ya mwananchi" alisema Juma


Shirika lisilo la kiserikali la Mwanasheria watetezi wa Mazingira kwa vitendo( LEAT) wametoa elimu ya Mazingira kwa miaka minne mfululizo hivyo Vijiji vyote vya mradi ambavyo vipo wilaya ya iringa na wilaya ya Mufindi na kuiomba serikali kuendelea kuboresha Mazingira ambayo yapo chini yao.


Franklin Masika ni Afisa ughani wa shirika la LEAT aliwataka wananchi kufuata sheria ya mazingira mwaka 2004 namba 20 na sheria ya maji ya mwaka 2009 namba 11 zinaeleza wazi kuhusu kilimo cha vinyungu au kulima kandokando ya mto au kwenye vyanzo vya maji na kuna faini zimeolodhishwa hivyo sheria hizi sio ngeni ili zilikuwa hazifuatwi lakini saizi serikali imeanza kuzifuatilia kwa umakini zaidi.


"Mkiangalia nyie hapa kijiji cha uhambila kipo katika bonde la mto rufiji hivyo wananchi mnatakiwa kuwa makini na hizi sheria kwa kuwa lengo la serikali ni kuboresha Mazingira ya kuukuza mto ruaha mkuu ambao unahati hati ya kutoweka na nyie ni walinzi namba moja wa Mazingira "alisema Masika


Lakini Franklin Masika aliztaja baadhi ya adhabu zinazotokana na uharibifu wa Mazingira mfano kuchepusha maji,kukinga,kuchukua au kutumia maji kinyume cha sheria ni kosa la jinai na adhabu yake ni shilingi 300,000 na isiyozidi 500,000 au kifungo cha miezi miwili na kifungo kisichozidi miezi sita au vyote viwili kwa pamoja hivyo wananchi wanapaswa kuwa makini na hizo sheria.


Masika aliwataka wananchi wa kijiji cha uhambila kuwa kutunza vyanzo vya maji na Mazingira kwa ujumla ili kuboresha maeneo wanayoishi na kupunguza au kufuta Kabisa milipuko ya magonjwa ilanayotokea mara kwa mara katika maeneo ya Vijijini.


Chelsoni Kikoti, Amani Nyakunga na Reginandi Chalamila ni wananchi wa kijiji cha uhambila waliiomba serikali zitafakali upya sheria hizo kwa kuwa zinawaumiza wananchi wa vijijini kutokana na Mazingira wanayoishi kutokuwa rafiki na namna ya kupata kipato hivyo wemekuwa wakitegemea sana kilimo cha mboga mboga kuendesha maisha yao.


"Hebu angalieni Mazingira haya tunayoishi hakuna njia nyingine ya kupata kipato zaidi ya kutegemea kulima vinyunguni ambako tunalima mboga mboga tu jamani hee tuatakufa na njaa hebu muishauri serikali juu sheria hizo"walisema wananchi


Thomas Mtelega afisana mradi wataasisi ya mufindi kwa maendeleo (MUVIMA) aliwaomba wananchi kulima Kilimo cha kisasa kutokana na Mazingira wanayoishi na kuacha tabia za kukata miti pamoja na kuharibu vyanzo vya maji mfano kulima mboga mboga ni rahisi unaweza kulima hata kwa kutumia maji.


"Kuna maji machafu ambayo tunayoyatumia majumbani kwetu ni maji ambayo tunaweza kuyatumia katika Kilimo cha mboga mboga kwa kuchukua udongo na kuuweka kwenye gunia au visarufeti ambavyo ukipanda mbegu unaweza kupata mboga nzuri na salama kwa kuwa guni au kisarufeti kinaweza kujchuja uchafu wote na kuiacha mboga ikiwa salama hivyo nawashauri wananchi kutumia njia hii ili kuondokana na ulimaji wa karibu na vyanzo vya maji na kusababisha Mazingira yanaboresha na kuwa mazuri"alisema Mtelega

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha uhambila Agnes Simba aliwashukuru shirika la LEAT kwa elimu waliyokuwa wanantoa kwa miaka nne ambayo imewakomboa wananchi kwa kupata vitu vingi ambavyo sasa vimeanza kutokea na vinakuwa sio vigeni hasa maswala ya sheria za Maliasili na utunzaji wa vyanzo vya maji ambavyo vinafaida kwa wananchi wa sasa na baadae.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...