Skip to main content

WALIMU WAISHI KATIKA NYUMBA MOJA


Wanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Nyakadete iliyopo Kijiji cha Nyakadete Kata ya Madibira wilayani Mbarali, mkoani Mbeya wakimsalimia mgeni alipoingia darasani kwao hivi karibuni. (Picha na Friday Simbaya)


Shule ya Msingi Nyakadete iliyopo Kijiji cha Nyakadete Kata ya Madibira wilayani Mbarali, mkoani Mbeya inakabiliwa na uhaba wa nyumba za walimu na kupelekea baadhi ya walimu kuishi katika nyumba za familia za walimu wengine, imefahamika.

Hivi karibuni Nipashe ilitembelea shule hiyo na kubaina kuwa kuna nyumba tatu (3) tu za walimu wakati mahitaji ni nyumba tisa (9).

Kutokana na hali hiyo walimu wanalazimika kuishi kilometa 12 toka shuleni, kwa mfano mwalimu anatoka Kijiji cha jirani cha Mkunywa kilichopo katika Kata ya Madibira, wilayani Mbarali.

Walimu wengine wanaishi katika nyumba za familia ya mwalimu mwingine, yaani mwalimu kuwa kama sehemu ya familia ya mwalimu mwingine.

Meshack Salehe ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyakadete, alithibitisha uwepo wa hali hiyo, na kusema kuwa wapo baadhi ya walimu wanaoishi katika familia ya mwalimu mwingine kutokana na uhaba wa nyumba za walimu shuleni hapo.

Nipashe pia ilibaini kwamba shule hiyo pia inaupungufu wa vyumba vya madarasa na ukosefu wa maji safi na salama kutokana na kuaribika kwa kisima cha maji kwa muda mrefu.

Kutokana na hali hiyo ya kutokuwepo maji, wanafunzi wanatumia muda mwingi kutafuta maji toka mitaani na kupelekea kukosa muda wa masomo.

“Wanafunzi hawana muda wa michezo kwa sababu muda mwingi wanatumia kutafuta maji yatumia wao wenyeww na wakati mwingi ya walimu,” alisema Salehe.

Alitaja changamoto zingine kuwa ni kukosekana kwa maji ambapo kumechangia kuwafanya watoto wa kike kuwa katika wakati mgumu hasa wanapokuwa kwenye hedhi.

Alisema matatizo mengi ya miundombinu ambayo huathiri zaidi watoto wa kike, yanatokana na changamoto za mfumo wa bajeti ya sekta ya elimu, hivyo suala la kuboresha miundombinu ya shule linapaswa kuwa kipaumbele zaidi kwa kuongeza fedha za bajeti ya maendeleo.

Shule hiyo inakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya kufundishia somo la Teknolojia ya Habari na Mawsiliano (Tehama) kama vile kompyuta na kulazimisha mwalimu wa somo hilo kuchora ubaoni wakati wa kipindi cha somo hilo.

“Somo la Tehama ni somo muhimu katika shule zote za msingi na Sekondari ukizingatia wakati huu wa sanyasi na teknolojia ili kukidhi mahitaji ya dunia ya sasa, hasa kwa nchi yetu Tanzania,” alisema mwalimu mkuu.

Alisema kuwa TEHAMA imebakia katika nadharia tu, kwani walimu wengi wanaofundisha somo hili hawana vifaa vya kufundishia somo hilo na kupelekea mwanafunzi kutoelewa kinachoendelea darasani.

“Somo hili linabakia kukariri msamiati mgumu wa taaluma hii ili mwanafunzi aweze kujibu maswali atakayoulizwa katika mtihani na siyo kumwandaa kwa kuitumia taaluma hii katika maisha yake ya sasa na baadae.,” alisisitiza mwalimu mkuu.

Shule ya msingi Nyakadete ilianza mnamo tarehe 29/06/2004 ina wanafunzi zaid 250, na imeongozwa na walimu wakuu saba (7) tangu kuanzishwa kwake.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...