Skip to main content

Watumishi Sita Manispaa Ya Iringa Wafukuzwa Kazi Kwa Utoro


Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Alex Kimbe akifungua kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu ya mwaka 2016/2017 wa halmashauri hiyo leo unaofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)


Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Alex Kimbe akimkabidhi mmoja ya watumishi wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Musa Mwaihojo (kulia) cheti cha pongezi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri hiyo, ikiwa ni pamoja na ushuru wa mabango na leseni wakati wa kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu ya mwaka 2016/2017 wa halmashauri hiyo leo unaofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)


BARAZA la Madiwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa limewafukuza kazi watumishi wake sita na kumrudisha kazini mmoja kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo utoro kazini.

Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe, ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la madiwani aliwataja watumishi hao waliokumbwa na adhabu hiyo kwa utoro kazini kuwa ni Glory Ngowi, Anzawe Mvena, Francis Mtenge, Paul Sanga, Mkombozi Gendagenda na Tumaini Sanga.

Kimbe alikiambia kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Iringa jana (Jumamosi) kuwa watumishi hao sita (6) wamefukuzwa kazi kutokana na kutokuwepo kwenye vituo vyao vya kazi bila taarifa yoyote.

“Watumishi hawakuwepo kazini kwa zaidi ya miaka miwili na wamefukuzwa kutokana na kutokuwepo kazini kwa zaidi ya miaka miwili bila ruhusa ya mwajiri wake kinyume na Kanuni za Utumishi wa umma za mwaka 2003, na kuanzia leo tarehe 20 mwezi Mei, mwaka 2017 watajwa hapo juu sio watumishi wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa,” alisema Kimbe.

Aidha, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani huyo alisema kuwa halmashauri hiyo imemrudisha kazini Lucy Mtafwa baada ya kamati kuridhia kuwa hakutenda makosa ya kiutumishi na hatimaye baraza lilipendekeza mtumishi huyo arudishwe kazini. 

Wakati huo huo, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imekusanya zaidi ya shilingi milioni 400 (400m/-) kodi ya mapato kwa mwezi Machi mwaka 2017.

Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe kwa kutambua mchango wa usimamizi wa ukusanyaji kodi aliwatunuku vyeti vya pongezi vya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri baadhi ya watumishi waliosimamia zoezi hilo.

Akiongea wakati wa kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu ya mwaka 2016/2017, meya huyo alisema mapato hayo ni kutokana na ushuru wa mabango na leseni.

Kikao cha baraza la madiwani halmashauri ya Manispaa ya Iringa cha robo ya tatu ya mwaka 2016/2017, kilikaa na kujadili taarifa mbalimbali za miradi ya maendeleo pamoja kuwafukuza kazi watumishi sita kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo utoro kazinina kumrudhi mmoja kazini.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...