Skip to main content

HABARI KUHUSU UTAMBUZI NA USAJILI WA WAKAZI WA MANISPAA YA IRINGA


Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa tumeanza zoezi la Kutambua na Kusajili wakazi wa Manispaa ya Iringa.
Zoezi limeanza tarehe 07/06/2017 na linatarajiwa kukamilika tarehe 05/07/2017. Zoezi linaanza saa 1 asubuhi hadi saa 11 Jioni. Zoezi litafanyika katika Vituo vya Usajili vilivyopo katika Kata zote 18 za Manispaa ya Iringa kwa mujibu wa Ratiba ilivyopangwa kila Kata imepangiwa siku 3 za usajili.   

Zoezi za usajili litahusisha wananchi wote raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.

Vitu vya Msingi anavyotakiwa kwenda navyo Mwananchi Raia wa Tanzania katika kituo cha usajili ni:-

1.   Nyaraka halisi (original) na vivuli vya kuthibitisha uraia na umri wa Mhusika,
2.   Cheti cha Kuzaliwa,
3.   Pasi ya Kusafiria,
4.   Vyeti vya Elimu ya Msingi na Sekondari,
5.   Leseni ya Udereva,
6.   Kitambulisho cha Bima ya Afya,
7.   Kitambulisho cha Mpiga kura.

Kwa kuwa zoezi hili linahusisha upigaji wa Picha, kwa ajili ya ubora wa picha, Tunaelekeza yafuatayo kwa wananchi:-
· kutovaa nguo Nyeupe, Kijivu, Bluu mpauko, Pinki, nguo zenye kung’aa sana, Jezi, nguo zenye nembo, kofia aina yeyote ama kupaka Hina mikononi.

Matarajio katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ni kusajili wakazi 130,000 kwa ajili ya Vitambulisho vya Taifa.

Mwananchi jitokeze Usajiliwe ili Upate Kitambulisho cha Taifa kwa Maendeleo yako na Taifa kwa Ujumla
Imetolewa na:

Dennis Gondwe,
Afisa Habari- Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
IRINGA8/6/2017 

RATIBA YA USAJILI KATIKA KATA NI KAMA IFUATAVYO:
SN
JINA LA KATA
TAREHE ZA USAJILI
1
KITWIRU
7-9/6/2017
2
RUAHA
7-9/6/2017
3
IGUMBILO
10-12/6/2017
4
MSHINDO
10-12/6/2017
5
KITANZINI
10-12/6/2017
6
MIVINJENI
10-12/6/2017
7
MLANDEGE
13-15/6/2017
8
KWAKILOSA
13-15/6/2017
9
ILALA
13-15/6/2017
10
MWANGATA
18-20/6/2017
11
ISAKALILO
18-20/6/2017
12
MKWAWA
21-23/6/2017
13
MAKORONGONI
24-26/6/2017
14
GANGILONGA
24-26/6/2017
15
KIHESA
27-29/6/2017
16
MTWIVILA
30/6-02/7/2017
17
MKIMBIZI
30/6-02/7/2017
18
NDULI
3-5/7/2017


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...