Skip to main content

INTANETI INAVYOCHOCHEA UKUAJI WA UTALII BARANI AFRIKA


Na Jumia Travel Tanzania

Afrika ni bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu ambapo inafikia takribani bilioni 1.2 (wengi wao wakiishi mijini) na inatarajiwa kongezeka mpaka bilioni 2.5 kufikia mwaka 2050 (25% ya watu wote duniani).




Kwa mujibu wa ripoti ya utalii kwa Afrika mwaka 2017 iliyofanywa na Jumia Travel imebainisha kwamba mtu mmoja kati ya watatu ni sehemu ya watu wa daraja la kati (watu wanaofanyakazi kwenye taaluma na biashara mbalimbali pamoja na familia zao) na wanatarajiwa kuongezeka mara mbili zaidi kufikia 2050. Watu wa daraja la kati ni muhimu katika uchangiaji wa ukuaji wa utalii wa ndani na ukanda mzima tuliopo.


Miongoni mwa mambo yanayochochea maendeleo na ukuaji wa sekta mbalimbali Afrika ikiwemo utalii ni pamoja na mtandao wa intaneti.


Mpaka hivi sasa, watumiaji wa mtandao wa intaneti barani Afrika wamefikia zaidi ya milioni 300, ambayo ni sawa na 9.3% ya waafrika wote na 27.7% ya ueneaji wake. Kwa kiasi kikubwa idadi hiyo imechangiwa na kuingia na kuongezeka kwa matumizi ya simu za mkononi.




Ripoti hiyo imeendelea kufafanua kuwa mnamo mwishoni mwa mwaka 2015, 46% ya waafrika walijiunga na huduma za simu za mkononi. Na idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka kufikia milioni 725 kufikia mwaka 2020. Na hiyo imetokana na upatikanaji wa mtandao wa intaneti wa 4G kwa zaidi ya nusu ya nchi za kiafrika, ambapo mpaka kufikia katikati ya mwaka 2016 takribani nchi 32 zilikuwa zimekwishaunganishwa na mitandao 72 ya LTE (Long-Term Evolution). 


Kutokana na maendeleo hayo ya matumizi ya intaneti, sekta ya utalii hususani huduma za hoteli na malazi kwa ujumla inanufaika kwa kiasi kikubwa. Na hii ni kutokana na wateja kuwezeshwa kufanya kila kitu wakiwa mtandaoni badala ya kutembelea moja kwa moja hotelini.


Jumia Travel kwenye ripoti yake imebainisha kwamba idadi kubwa ya wateja wanatafuta na kufanya huduma za hoteli mtandaoni kwani ni salama, haraka na uhakika zaidi. Ripoti inaonyesha kwamba wateja wengi hutafuta huduma mtandaoni kwa kutumia simu za mkononi (51%) zaidi ukilinganisha na kompyuta (49%). Vivyo hivyo pia kwenye kufanya huduma yenyewe wengi hupendelea zaidi simu za mkononi (68%) dhidi ya kompyuta (32%).


Takwimu hizo ni ishara nzuri kwamba waafrika wamekubali kuyapokea mabadiliko yaliyotokana na mtandao wa intaneti hususani kwa matumizi yenye faida kwao. Kwa hiyo ni fursa kwa wadau wa sekta ya utalii kujikita zaidi mitandaoni ili kuweza kuendana na kasi ya wateja wengi wanaohamia huko.




Ingawa bado tupo nyuma kwa kiasi fulani ukilinganisha na mabara mengine lakini hali imebadilika ukilinganisha na kipindi cha nyuma. Hivi sasa, wasafiri wengi kutokana na kurahisishiwa kila kitu mtandaoni imekuwa ni rahisi kwao kufanya huduma wakiwa mahali popote na muda wowote.


Kwa mfano, wateja wengi wanaitumia njia ya mtandao kufanya huduma zao za malazi tofauti na hapo awali ambapo ilibidi kupiga simu au kwenda moja kwa moja hotelini. Mtandaoni kuna orodha ya hoteli zote, zikiwa sehemu moja, zikionyesha mahali zilipo, bei za vyumba vyake, upatikanaji wake na pia namna ya kufanya malipo. Hivyo kumrahisishia mteja kwa kuokoa muda na gharama ambavyo vingepotea kwa kutembelea hoteli moja kwenda nyingine.


Mtandao wa intaneti si tu umewarahisishia wateja kupata huduma kwa urahisi na uhakika lakini pia hata mameneja wa hoteli na wapokea huduma. Kwa mfano, kwa sasa kuna mifumo ambayo inawawezesha kuratibu mwenendo na utaratibu wa shughuli zao mahali popote walipo na muda wowote wautakao.


Mfumo huo huwarahisishia kupokea na kuthibitisha upatikanaji wa huduma, kuwa na uhakika na idadi ya vyumba walivyonavyo, kujua idadi na aina ya wateja wanaopendelea huduma zao pamoja na kupokea maoni mbalimbali juu ya huduma wanazozitoa. 



Ripoti hiyo pia imebainisha kwamba orodha ya nchi nane ambazo ueneaji wake wa mtandao wa intaneti ni mkubwa barani Afrika ni kama vile; Kenya (74%), Mauritius (63%), Shelisheli (57.6%), Morocco (57.3%), Nigeria (52%), Afrika ya Kusini (51.6%), Tunisia (50.5%) na Cape Verde (44.1%). 






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...