Skip to main content

Sheria mpya ya ndoa, vizazi yaja






SERIKALI kupitia Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) inakamilisha mchakato wa kuwa na sheria mpya, itakayoendana na mabadiliko yanayotokea na kurahisisha na kuhamasisha usajili wa takwimu za matukio ya vizazi, vifo, ndoa na talaka ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Kabla ya hapo, muswada utawasilishwa bungeni ili sheria hiyo ipitishwe na baada ya hapo tuwe na sheria mpya. Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi alisema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa semina ya wahariri wa vyombo vya habari nchini, iliyohusu maboresho ya Mfumo wa Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu na Ukusanyaji wa Takwimu (CRVS) iliyofanyika mkoani Morogoro jana.

Profesa Kabudi alisema hali ya usajili na takwimu za matukio ya vizazi, vifo na sababu zake, ndoa na talaka sio nzuri, kwani idadi kubwa ya wananchi wamekuwa hawasajili matukio hayo yanapotokea, japo wengi wamekuwa na nia ya kufanya hivyo, lakini wameshindwa kutokana na sababu mbalimbali.

Alisema wananchi wengi wamezaliwa na kufariki bila ya kuwepo kwenye kumbukumbu zao za matukio muhimu katika mfumo wa usajili wa kiserikali. “Wananchi hawa wanaishi lakini hawaonekani katika picha kubwa ya taifa inayochorwa kwa kutumia takwimu na sababu kuu ya kwa nini hawaonekani ni kwamba hawakusajiliwa wakati walipozaliwa,” alieleza Profesa Kabudi.

Aliongeza kuwa kumekuwepo na sababu mbalimbali, zinazochangia hali hiyo nchini na kati ya hizo ni umbali uliopo kutoka kwenye vituo vya tiba, ambapo usajili wa vizazi hufanyika kwa mtoto anapozaliwa.

Alisema wazazi hulazimika kusafiri umbali mrefu kwenda eneo la kuwasilisha maombi ya kumpatia mtoto cheti cha kuzaliwa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Hivyo alisema kutokana na changamoto hizo, wananchi wengi wamelazimika kutowasajili watoto wao na hivyo kuongeza mlundikano wa wananchi wasio na vyeti vya kuzaliwa nchini.

Pamoja na hayo, alisema takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012, zilionesha kuwa asilimia 13.4 ya wananchi ndio wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa. Alisema hiyo ni idadi ndogo na ni kiashiria kuwa serikali haina taarifa za idadi kubwa ya wananchi.

Alieleza kuwa serikali kwa kulitambua tatizo hilo, tayari imeanza kuchukua hatua kwa kufanya maboresho ya mfumo wa usajili uliopo na kuanzisha mfumo utakaofanya kazi vizuri ili kusajili matukio muhimu ya binadamu na takwimu (CRVS).

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya RITA, Profesa Hamis Dihenga kabla ya kumkaribisha waziri kufungua semina hiyo, alisema Rita ina wajibu wa kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kusajiliwa ili nchi iwe na idadi kamili ya watu wake kwani kwa sasa asilimia 87 ya Watanzania hawajasajiliwa na hiyo ni idadi kubwa.

Profesa Dihenga alisema ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha anakuwa na taarifa zake kikamilifu; hivyo alisema elimu zaidi inaendelea kutolewa kwa wananchi na kuelezea pia changamoto za mfumo na sheria zilizopitwa na wakati ambazo zimekuwa zikichangia kukwama kufikiwa kwa baadhi ya mambo. CHANZO: HABARILEO

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...