Skip to main content

Unywaji maziwa bado tatizo mkoani Iringa


Walimu wa shule ya Msingi JJ Mungai Manispaa ya Iringa mkoani Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wao baada ya kupewa mgao wa maziwa na Kampuni ya Asas Dairies Ltd ya mjini Iringa jana.




Watanzania waliungana na wenzao katika kuadhimisha Wiki ya Unywaji Maziwa ambapo kilele cha maadhimisho kilikuwa juni mosi mwaka huu.


Katika maadhimisho hayo, imebainika kuwa Watanzania bado wako nyuma katika unywaji wa maziwa ikilinganishwa na nchi nyingine kama vile Kenya.


Meneja wa miradi wa Asas Group of Companies Ltd Hassan Swedi kwa upande amewataka wananchi kujenga utamaduni wa kupenda kunywa maziwa kila siku badala ya kusubiri wang’atwe na nyoka au wadudu kutoa sumu mwiilini ama washauriwe na madaktari.

alisema kuwa watu wengi wamekuwa wavivu katika suala la unywaji wa maziwa ikilinganishwa na kasi wanayoitumia kwenye unywaji wa pombe ambapo baadhi yao wamekuwa mabingwa wa kushinda au kukesha baa.

Akaongeza kuwa viwango vinavyopendekezwa kimataifa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) ni lita 200 kwa mtu kwa mwaka wakati unyanji wa maziwa kwa mtu ni lita 47 kwa mwaka kitaifa. 

Swedi aliwataka wananchi wa mkoani Iringa kuyatumia maadhimisho hayo kama darasa katika kujifunza mbinu bora za ufugaji wa ng’ombe wa maziwa na usindikaji wa maziwa kwa ajili ya kuinua kiwango cha upatikanaji wa maziwa hayo.

Kampuni ya Asas Dairies Ltd ilitumia maadhisho hayo kwa pakiti za 4,000 (sawa na lita 1,000) kwa wanafunzi wa shule mbali mbali za Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa .

Meneja wa miradi huyo alisema kuwa maadhimisha ya mwaka huu yamelenga zaidi vijana hasa wanafunzi wa shule za msingi mjini Iringa na ndio sababu kampuni yake imelazimika kutoa msaada wa maziwa kwa wanafunzi.

Alisema kuwa kampuni hiyo inaamini kuwa iwapo shule zitaweka utaratibu wa kuhamsisha unyanji wa maziwa kupitia kamati za lishe bora kwa wanafunzi afya za wanafunzi hao zitakuwa bora na kiwango cha elimu kinaweza kuongezeka zaidi mashuleni.

Mbali ya unywaji wa maziwa kuhamasishwa zaidi mashuleni bado viongozi wa serikali wanapaswa kuanza kuhamasha unywaji wa maziwa katika ofisi hizo za umma badala ya kutumia maziwa kutoka nje ya nchi .

Hata hivyo, mkoa wa Iringa unashika nafasi ya tatu kwa kuwa na watoto wenye utapiamlo kwa kuwa na asilimia 51.3 baada ya mikoa ya kagera (51.9)na Njombe wenye asilimia 51.5.

Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa inayoadhimishwa Kitaifa katika Mkoa wa Kagera katika Uwanja wa Kyakailabwa nje kidogo ya mji wa Bukoba kuanzia tarehe 28 Mei, 2017 hadi tarehe 1Juni, 2017. 

Malengo ya Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa inalenga kuelimisha wananchi na umma juu ya matumizi ya maziwa kama chakula bora kwa watu wa rika zote na faida za maziwa katika kujenga afya ya binadamu. 

Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo ni “Kunywa Maziwa Furahia Maisha“. Maadhimisho haya yatakuwa ya 20 mfululizo kuadhimishwa nchini ambapo yalianza kuadhimishwa kuanzia mwaka 1998 na mwaka jana yaliadhimishwa Mkoani Njombe. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...