Skip to main content

WAKINA BABA WATAKIWA KUTOA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA WATOTO WAO




Ofisa Programu wa TGNP Mtandao, Anna Sangai (kushoto), akitoa mada katika kongamano la siku moja lililohusu elimu ya afya ya uzazi lililofanyika Makao Makuu ya TGNP Mabibo Dar es Salaam jana. Kongamano hilo liliandaliwa na TGNP.



Mwanafunzi Leila Kisinga kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanamke vinavyofanya kazi.



Kongamano likiendelea.



Mshiriki Idd Hamisi akichangia jambo katika kongamano hilo.



Usikivu katika kongamano hilo.



Aisha Kijavara akichangia.



Wakina mama wakiwa katika kongamano hilo. Wakina mama hao walitoa uzoefu wao kuhusu afya ya uzazi kwa watoto.



Mwanafunzi Juma Nasoro kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanaume vinavyofanya kazi.



Mdau Selemani Bishagazi akichangia kuhusu wanaume kuwasaidia watoto wao wa kike wanapokuwa katika hedhi.



Mary Mbarawa akichangia jambo.




Na Dotto Mwaibale


WAKINA Baba nchini wametakiwa kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto wao badala ya kuwaachia kazi hiyo ifanywe na wakina mama pekee.


Mwito huo umetolewa na Selemani Bishagazi wakati akichangia mada katika kongamano la siku moja lililohusu elimu ya afya ya uzazi kwa watoto hasa wa kike lililoandaliwa na TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam jana.


"Suala la utoaji wa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto wetu hasa wa kike ni letu sote kati ya baba na mama kwani baba ndie chanzo kikubwa cha mapato katika familia" alisema Bishagazi.


Bishagazi alisema suala la kutoa fedha za kunulia pedi wakati mtoto wa kike anapokuwa kwenye hedhi si la mama bali hata baba anawajibu wa kutoa fedha hizo na akaomba dhana hiyo potofu kuwa mama ndiye anawajibika katika suala hilo iachwe.


Alisema ni vizuri mtoto wa kike anapokuwa katika hedhi kuwajulisha wazazi wake ili aweze kusaidiwa kupata fedha za kununulia pedi badala ya kukaa kimya kwa hofu na kujikuta akishindwa kujistiri na kuchafuka.


Mshiriki mwingine katika kongamano hilo alisema usiri imekuwa ni changamoto kubwa katika kumsaidia mtoto kujua afya za uzazi kwani wazazi wengi wanashindwa kuwaweka wazi watoto wao kuhusu jambo hilo.


Alisema mtoto wa kike anapobalee na kuanza kuingia katika hedhi wazazi wanapaswa kumueleza kuwa amekuwa na hivyo iwapo atakutana na mwanaume atapata mimba hivyo kumpa elimu hiyo kwa wazi ataweza kujiepusha na kupata mimba badala ya kufanya siri.


Aisha Kijavara ambaye alishiriki katika kongamano hilo alisema ni vizuri elimu ya afya ya uzazi ikatolewa kwa uwazi na kutaja viungo vya uzazi bila ya kuona aibu ili watoto waweze kuelewa vizuri badala ya kufichaficha.


"Katika suala ili la utoaji wa elimu hii ya afya ya uzazi tunapaswa kuwa na muda wa kutosha na kutamka wazi viungo vya uzazi jinsi vinavyofanya kazi ili walengwa waweze kuelewa vizuri somo" alisema Kijavara.


Ofisa Programu wa TGNP Mtandao, Anna Sangai alisema wanapopigania bajeti zinazopitishwa na bunge ziwe na mlengo wa kutoa kipaumbele kijinsia zinamlenga zaidi mtoto wa kike ambao wanachangamoto nyingi hasa wale waliopo mashuleni kwani wengi wao hawana uwezo wa kununua pedi wanapokuwa katika hedhi.


Alisema baadhi yao wamejikuta wakiingia katika vishawishi vya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume ambao wamekuwa wakiwasaidia kuwanunulia bedi.


"Tumekuwa tukihimiza kutengwa kwa bajeti kubwa za wizara husika ili kuwasaidia watoto hawa ambao wapo katika changamoto hiyo" alisema Sangai.


Kongamano hilo lilihudhuriwa na Wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Mabibo ambao baadhi yao walitoa mada kuhusu afya ya uzazi na matumizi ya via vya uzazi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...