Skip to main content

CHODAWAU YATAKA WAAJIRI KUTOA MIKATABA KWA WAAJIRIWA



Katibu Mkuu Msaidizi wa Mkoa wa Iringa wa Chama cha Wafanyakazi wa Hifadhi, Hoteli, Majumbani na Huduma za Jamii na Kazi zinginezo (CHODAWAU), Silvester Mshana Mfumu amewataka waajiri mkoani hapa kuwalipa mikataba ya ajira wafanyakazi wao kabla ya sheria haijakuchua mkondo wake.

Alisema kuwa mkataba wa ajira ni makubaliano yanayofanywa na mtu au taasisi inayoitwa mwajiri kwa upande mmoja, na mtu anayefahamika kama mwajiriwa kwa upande mwingine kwa lengo la kuainisha haki na wajibu wa pande hizi mbili.

Kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, namba 6 ya 2004, mwajiri ni mtu au taasisi inayomlipa mtu mwingine ujira kwa ajili ya kutoa huduma, ujuzi au nguvu kazi inayofanikisha shughuli zake. 

Mshana alisema kuwa mwajiriwa, kwa upande mwingine, ni mtu mwenye sifa na uzoefu anayefanya kazi chini ya mamlaka ya mtu mwingine au taasisi akilipwa kwa minajili ya kutumia uzoefu na sifa .

Alisema kuwa mwaka wa fedha wa kiserikali umeanza na kuwataka waajiri kutoka sekta zinazohusu CHODAWAU kuwatapitia mikataba ya ajira waajirwa na wanachama kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini na Kanuni zake za Mwaka 2004.

Katibu msadizi huyo wa CHODAWAU alisema hayo jana wakati wa mahojiano maalum na NIPASHE na kuongeza kuwa kuwepo kwa mikataba hiyo kutasaidia kupunguza migogoro isio ya lazima pamoja na kuleta ufanisi katika kazi.

Mshana alisema kuna waajiri bado hawajanza kulipa kima cha chini cha mishahara baada ya serikali kupitia bodi ya mishahara iliyotangaza kwa sekta zote mwezi wa saba mwaka 2013.

Haki hizi ni pamoja na kupatiwa mkataba wa kazi, kufahamu ameajiriwa katika nafasi gani na majukumu yake ni yapi, ili asije akafanya majukumu yasiyomhusu. 

Alisema kuwa mfanyakazi ana haki ya kwenda likizo, kupatiwa likizo ya matibabu pamoja na likizo ya uzazi. 

Alisema kuwa kuna baadhi ya waajiri ambao bado hawajaanza kutekeleza agizo la Serikali la kupandisha mishahara ya wanafanyakazi kwa sekta binafsi kama ilivyopendekezwa na bodi ya mishahara nchini ya mwaka 2013.

“Tutaanza kuwahesabia waajiri mapunjo kwa wafanyakazi kwa wanachama wote wa CHODAWU kwa sababu Serikali kupitia bodi ya mishahara nchini litangaza viwango mbalimabli vya mishahara ikiwemo sekta binafsi, ambapo walitakiwa kuanza kulipa viwango hivyo kuanzia tarehe moja mwezi wa saba mwaka 2013, ” alifafanua Mshana.

Mfanyakazi ana haki ya kulipwa malipo stahiki yanayoendana na kazi anayofanya na kiwango kilichowekwa na Serikali kwa mujibu wa sheria. 

Sheria pia imeweka wazi wajibu wa mfanyakazi kuwa ni pamoja na kufanya kazi kwa bidii, kufikia malengo ya mwajiri, usiri, utii, nidhamu na uaminifu. 

“Msingi wa uhusiano wa kiajira baina ya mfanyakazi na mwajiri ni mkataba wa ajira. Mkataba wa ajira unaweza kuwa wa mdomo au wa maandishi. Ili kuhakikisha mambo ya msingi yanawekwa wazi Sheria inamtaka mwajiri kumpa mfanyakazi maelezo ya ajira yake kwa maandishi,” alisema Mshana

Waajiriwa wengi, hususani kwenye sekta binafsi, wanafanya kazi bila kuwa na mikataba. Utendaji na usalama wa wafanyakazi hawa, kwa kiasi kikubwa, unategemea hisani na uaminifu wa mwajiri.

Kufanya kazi bila mkataba kuna hatari kadhaa. Kwanza, panakosekana ushahidi wa kisheria kuwa umeajiriwa. Katika mazingira haya, inapotokea unapata matatizo kazini, itakuwa rahisi zaidi kupoteza kazi yako.

Vile vile, kutokuwa na mkataba kunakuweka kwenye hatari ya kupoteza haki zako za msingi kama mfanyakazi anayelindwa na sheria za nchi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...