Skip to main content

HATIMAYE LIPULI FC WAPATA VIONGOZI WAPYA


Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia FFU mkoa wa Iringa wakiwa wameweka ulinzi mkali ukumbi wa Shule ya sekondari Mwembetogwa mjini Iringa unaotumika kufanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa klabu ya Lipuli FC jana. (Picha na Friday Simbaya)

Mmoja ya viongozi wa Lipuli FC waliomaliza muda wao akitimiza haki yake yakuchagua viongozi wapya jana katika mkutano mkuu ya uchaguziwa klabu hiyo. (Picha na Friday Simbaya)


Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa timu ya mpira ya Lipuli wakifuatilia hotuba ya mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ambaye aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah jana. (Picha na Friday Simbaya



HATIMAYE Klabu ya soka ya Lipuli FC ya mkoani Iringa jana wamemchagua Ramadhan Mahano kuwa mwenyekiti mpya wa klabu hiyo baada ya kuwagalagaza wapinzani wake wawili. 

Katika uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya sekondari Mwembetogwa mjini Iringa na kushuhudiwa na mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ambae aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdallah.

Jumla ya wajumbe na wananchama 171 walishiriki mkutano mkuu wa uchaguzi wa klabu hiyo kongwe nchini na kuapata viongozi wapya watakayedumu kwa miaka mine ijayao. 

Akitangaza matokeo hayo ya uchaguzi huo Wakili Jackson Abraham Chakula alisema kuwa Mahano ameshinda kwa kura 103.

Wakati mpinzani wake Nuhu Muyinga akimfuata kwa kura 60 wakati Abnery Mrema akiambulia kura nne (4)tu.

Huku makamu mwenyekiti ambaye aligombea nafasi hiyo pekee yake Ayubu Kihwele akishinda kwa kura 116 huku kura zaidi ya 50 zikiharibika. 

Wajumbe wote wanne waliyogombea wamepita katika nafasi ya ujumbe wa kamati tendaji ambao ni Renatus Kalinga, Sylvester kanyika, Shaban Lushino na Magid Matolla. 

Awali mgeni rasmi katika mkutano huo mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abudallah aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi watakao ifanya Lipuli kusonga mbele na sio viongozi wa kuendekeza migogoro na kurudisha nyuma Lipuli. 

Alisema kwa kupitia Lipuli FC mkoa wa Iringa utaweza kupiga hatua ya kimaendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya utalii katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha na maeneo mengine mengi ya utalii mkoani Iringa. 

Kwa upande wake aliyekuwa mwenyekiti wa Lipuli FC Abuu Changawa alisema amepisha uchaguzi huo yeye na wenzake ili timu hiyo kusonga mbele na iwapo watashindwa kufanya vema basi atafanya mapinduzi kuwaondoa viongozi hao.

Naye Mwenyekiti Mpya wa Lipuli Ramadhan Mahano aliwapongeza wanachama wa Liupuli kwa kutumia demokresia ya kuchagua viongozi wao.

“Tunaomba tupige kazi ya kuiletea Iringa heshima ya mpira kwa wanairinga wote wana kiu kubwa ya mpira…,” alisema Mahono.

Aidha mwenyekiti mpya huyo aliwataka wapinzani wake wazidi kushirikiana naye katika kuinua soka la Lipuli ili iwatangaze kitaifa na kimataifa.

Mahano waliwaomba wanachama na wadau wa soka ndani na nje ya Iringa kuungana kuisapoti timu na uongozi uliopo madarakani kwa kuwa wamechaguliwa kidemokrasia.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...