Skip to main content

MWIGULU AKEMEA SIASA ZA KISHAMBA NCHINI


Na Friday Simbaya, Iringa

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Lameck Nchemba amesema Tanzania bado kuna ulimbukeni wa demokrasia kwa kubaguana katika misingi ya vyama vya siasa.

Mwigulu alitoa kauli hiyo jana (JUMAPILI) wakati akitoa salamu za serikali katika ibada maalum ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Mlandege katika Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa. 

Alisema kuwa bado anashangaa kuona watu wanabaguana kwa itikadi ya vyama pamoja na siasa ya vyama vingi nchini kudumu kwa miaka zaidi ya 20 sasa.

“Inatakiwa watu tuwe tunataniana kama tunavyotaniana kwenye mpira na ndugu yangu DC Kasesela kuhusu Singida united na Lipuli FC au mpira wa Yanga na Simba…,” alisema Mwigulu.

Mwigulu aliambatana na mwenyeji wake Richard Kasesela ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa.

Aidha, ibada hiyo iliongozwa na Askofu wa Dayosisi ya Iringa Blaston Tuluwene Gaville akisaidiana na mchungaji kiongozi Rhodeni Mang'lisa. 

Pia ibada hiyo ilikwenda sambamba na changizo (harambee) kwa ajili ya ujenzi wa kanisa unaoendelea wa Usharika wa Mlandege, ambapo Mwigulu alichangia shilingi milioni tano na kuahidi kutoa bati 600 kwa kuezekia kanisa hilo.

DC Kasesela na pia alichangia pesa taslimu shilingi milioni moja kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo unaondelea.

Alisema kuwa anashangaa kuona bado watu wanafanya siasa za kishamba katika misingi ya vyama vya siasa na kuongeza kuwa huku nikuonesha kwamba Tanzania demokrasia bado haijakomaa.

“Watu wanauana kwa sababu za vyama vya siasa kumbe walitakiwa kufanya kazi kwa pamoja kama ndugu wa taifa moja lakini sio kutoana roho kwa misingi ya vyama, huo ni ushamba wa kidemokrasia…,” alisema Mwigulu. 

Mwigulu alisema kuwa waumini wa madhehebu ya dini mbalimbali wanawajibu mkubwa wa kuwa pamoja na wakati wote kwa kumuombea dua na sala rais dkt John Pombe Magufuli kila siku ili aweze kufanikiwa.

Naye mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kanisa Boas Danford alisema kuwa wanahitaji zaidi ya shilingi milioni 75 kukamilisha ujenzi huo, ambapo tayari wameshatumia shilingi milioni 78,468,000/-.

Alisema kuwa kanisa hilo litakuwa ni la ghorofa moja lenye uwezo la kubeba washarika jumla ya 1,100 pamoja na ofisi za usharika ndani yake.

Danford alisema hadi kukamilika kwa ujenzi huo litagharimu shilingi milioni 350/- na kuongeza kuwa tangu kuanza kwa ujenzi huo hakuna msaasa wowote kutoka nje isipokuwa ni michango mbalimbali kutoka kwa washarika.

Aidha, Usharika wa Kanisa la Mlandege lilianzinshwa mnano 24.10.1983 ikiwa na washarika 120 tu lakini washarika wameongeza na kufikia 1,950, ambalo kwa sasa kanisa hilo linaongozwa na mchungaji kiongozi Rhodeni Mang’ulisa.

Hadi tuanenda mitamboni mchango na ahadi ziliendelea kutoa na wageni waarikwa  na waumini mbalimbali ambapo pia Askofu wa Dayasisi ya Iringa naye aliahidi kutoa shilingi milioni one na ishrini.



Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...