Skip to main content

TANZANIA YA UCHUMI WA VIWANDA ITAFANIKIWA KWA KUFUATA KILIMO CHA KITAFITI NA TAFITI




Mkuu wa Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Geofrey Ngupula akizungumza na maofisa ugani na waandishi wa habari wilayani humo leo, wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya maofisa ugani yalioandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa la Bioteknojia (OFAB), yenye lengo la kuwakumbusha wataalamu hao wa kilimo nafasi yao pamoja na kuwapatia mbinu mpya za kisasa katika kulima mazao ya Mihogo, Pamba na Viazi lishe katika kuelekea serikali ya viwanda. Kulia ni Katibu wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) wa wilaya hiyo, Arafa Njechele na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, Kiwele Michael.





Mkuu wa Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Geofrey Ngupula akizungumza na maofisa ugani na waandishi wa habari ofisini kwake.


Kaimu Mkurugenzi wa wilaya hiyo Hadija Kabojela akizungumza katika mafunzo hayo.



Mtafiti wa Kilimo kutoka COSTEC, Bestina Daniel akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH.



Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Onesmo Kisoka akizungumza kwenye mafunzo hayo.





Mshauri wa masuala ya Bioteknolojia kutoka Jukwaa la Bioteknolojia (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange akitoa mada kuhusu umuhimu wa matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo.






Mratibu wa Jukwaa la Biotehnolojia kwa maendeleo ya kilimo nchini (OFAB), Philbert Nyinondi akitoa ufafanuzi wakati wataalamu hao wa kilimo walipokuwa wakijitambulisha kwa mkuu wa wilaya.



Maofisa Ugani wakiwa katika mafunzo hayo.



Mafunzo yakiendelea.



Usikivu katika mafunzo hayo.



Maofisa Ugani ndani ya mafunzo.





Mratibu wa Jukwaa la Biotehnolojia kwa maendeleo ya kilimo nchini (OFAB), Philbert Nyinondi, akiteta jambo na Mtafiti wa kilimo, Bestina Daniel. 






Meza Kuu.



Taswira ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega wakati wa mafunzo hayo.




Hapa mafunzo yanaendelea. 



Picha ya pamoja na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Nzega, mbele alievaa kaunda suti.




Na Dotto Mwaibale, Nzega




TANZANIA ya Viwanda itafanikiwa kwa kuzingatia kilimo cha kitafiti na tafiti za watalaamu na kuachana na kilimo cha mazoea.


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Geofrey Ngupula wilayani humo leo asubuhi wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya maofisa ugani wa wilaya hiyo yalioandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa la Bioteknojia (OFAB), yenye lengo la kuwakumbusha wataalamu hao wa kilimo nafasi yao pamoja na kuwapatia mbinu mpya za kisasa katika kulima mazao ya Mihogo, Pamba na Viazi lishe katika kuelekea uchumi wa viwanda nchini. 

Alisema kuwa inaaminika kuwa zaidi ya asilimia sabini na tano ya watanzania ni wakulima huku zaidi ya robo tatu wakilima kimazoea na kutokana na mabadiliko ya tabia nchi kilimo kinaendelea kumdidimiza mkulima na kukifanya kilimo kuajiri 

idadi kubwa ya mafukara.


Alisema Teknolojia ya Uhandisijeni (GMO) inafanya vizuri duniani kote hivyo nchi inatakiwa kuitekeleza ili kuyafikia mapinduizi halisi ya kilimo katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi yanayo leta ukame, magonjwa na wadudu sugu wahalibifu wa mazao.

Katika hatua nyingine Ngupula aliwataka maofisa ugani kubadilika ili kuendana namabadiliko ya teknolojia ya kilimo katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kilimo.

Akizungumza wakati akitoa mada kwa maofisa ugani hao kuhusu matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo Mshauri wa masuala ya Bioteknolojia kutoka Jukwaa la Bioteknolojia (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange alisema teknolojia hiyo imeleta mapinduzi 

ya kilimo kwa nchi ambazo imeanza kuitumia hivyo wakati sasa ufike wa kuanza kuitumia hapa nchini.


Kaimu Mkurugenzi wa wilaya hiyo Hadija Kabojela aliwaomba watafiti wa kilimo kuzalisha kwa wingi mbegu za mhogo ili ziwafikie wakulima kwa wakati wakati wa msimu wa kilimo hicho.

"Kunachangamoto kubwa ya kupata mbegu bora hivyo ni vizuri mbegu zilizofanyiwa utafiti katika vituo vya utafiti zikawafikia wananchi kwa wakati jambo litakalosaidia wakulima kuacha kutumia mbegu duni zisizo na tija" alisema Kabojela.


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Mtafiti wa Kilimo, Bestina Daniel alisema mafunzo hayo ni moja ya utekelezajiwa kazi za COSTECH za kuwawezesha wakulima na wagani katika kutumia mbinu na teknolojia bora za kilimo kwenye uzalishaji ili kuongeza tija na 

kupunguza umasikini kwenye kaya.

Alisema Costech ndio wenye dhamani ya kuishauri Serikali kwenye masuala yote yanayohusu Sayansi na Teknolojia hivyo pale kunapotokea teknolojia na mbinu nzuri 

ambazo zinaweza kuleta mageuzi kwenye uzalishaji kwa wakulima hutafuta mbinu mbalimbali za kuzifikisha kwa wahusiaka.


Aliongeza kuwa ili kufikia kwenye uchumi wa viwanda lazima malighafi za kutosha ziwepo ili kulisha viwanda hivyo na kuzalisha bidhaa hivyo mazao hayo ambayo 

Costech inayahamasisha yatasaidia sana katika kulisha viwanda vya nguo,usindikaji wa mihogo na viazi lishe ambavyo vina umuhimu mkubwa kwenye kuongeza lishe na usalama wa chakula.



Mafunzo hayo ya siku moja kwa maofisa ugani hao yanalenga kuwapatia mbinu bora za uzalishaji wa mazao ya Mihogo,Viazi lishe pamoja na Pamba na nafasi ya matumizi bioteknolojia kwenye kuongeza uzalishaji na kutatua changamoto za kilimo kama magonjwa,wadudu na matatizo ya mabadiliko ya tabia nchi.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...