Skip to main content

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA IRINGA LAPATA NAIBU MEYA MPYA



Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Dr.William D. Mafwere (kulia) akizungumza wakati BARAZA Maluum la Madiwani la Manispaa ya Iringa mkoani Iringa jana. Kulia kwake ni Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe na Naibu Meya mpya limemchagua Daddy Igogo Diwani wa kata ya Gangilonga. (Picha na Friday Simbaya)


BARAZA la Madiwani la Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa limemchagua Daddy Igogo Diwani wa kata ya Gangilonga kuwa Naibu Meya mpya wa kwa kura 15 kati ya 26.

Igogo aliyekosa mpinzani baada ya diwani wa kata ya Nduli kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Bashiri Mtove kujitoa katika kinyang’anyiro hicho alishinda kwa kupata kura 15 na kunyimwa kura 11 kati ya kura 26 zilizopigwa.

Uchaguzi huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Iringa tarehe 10.08.2017 siku ya Alhamisi na uliudhuriwa na wajumbe 26 waliopigakura, ambapo mgombea huyo ameshinda kwa kupata kura 15 za ndio huku kura 11 kati ya 26 zikiwa ni hapana.

Kwa ushindi huo, Igogo anavaa viatu vya Diwani wa Kata ya Kwakilosa, Joseph Lyata (Chadema) aliyekuwa Naibu Meya katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Halmashauri ya Manispaa ya Iringa inaundwa na madiwani 28 kati yao Chadema ina madiwani 21 (14 wa kuchaguliwa, watano wa viti maalumu na wabunge wawili-Mchungaji Peter Msigwa ambaye ni mbunge wa jimbo la Iringa Mjini na Suzan Mgonakulima mbunge wa viti maalumu).

Na CCM ina madiwani saba ( wanne wakuchaguliwa, viti mmoja na wabunge wawili wa viti maalumu Rita Kabati na Zainabu Mwamwindi) 

Aidha, Naibu Meya huyo ameshukuru wajumbe wote walioudhulia katika Uchaguzi huo kwa kumuamini na kumchagua kuwa Naibu Meya. Pia ameomba ushirikiano kwa wajumbe na Viongozi wa juu kwa siku zijazo.

Mbali na hayo Baraza hilo limefanya uteuzi mpya wa Wenyeviti wa kamati tano za kudumu za Manispaa ikiwemo kamati ya Fedha na Uongozi ambayo itaongozwa.

Alex Kimbe,Kamati ya Mipangomiji na Mazingira itaongozwa na Tandessy Sanga,Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu ambayo itaongozwa na Raphael L. Ngullo, Kamati ya kudhibiti Ukimwi itakayoongozwa na Daddy Johanes Igogo na Kamati ya Maadili itaongozwa na Severin J. Mtitu.



Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...