Skip to main content

DC KILOLO AMSIMAMISHA KAZI MWENYEKITI WA KITONGOJI CHA ITUNGI


Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Itungi wilayani Kilolo, mkoani Iringa wakifuatilia mkutano wa hadhara wa kitongoji hicho uliohudhuria na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abadallah hayuo pichani juzi. (Picha na Friday Simbaya)

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Abdallah amewasimamisha kazi mwenyekiti wa kitongoji cha kitongoji cha Itungi ilikupisha uchunguzi kwa tuhuma zinazomkabiri kutokana na kushindwa kusimamia shughuli za maenedeleo katika kitongoji hicho.

DC huyo wamefikia hutua hiyo juzi katika mkutano ya hadhara ulioitisha na kitongoji hicho baada ya kuwepo na mgogoro wa uongozi kati ya Kata ya Mlafu na mwenyekiti wa kitongoji hicho katika mamlaka ya mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo, mkoani Iringa.

Alisema kuwa mnamo mwaka 2014 Kata ya Mlafu iliweka mipango ya ujenzi wa bweni na ukarabati wa maabara katika shule ya sekondari Mlafu.

Hivyo kila kitongonji kilipangiwa malengo ya kukusanya fedha kulingana na idadi ya nguvu kazi, hivyo kwa miaka mine sasa kitongoji hicho hakijafanya maendeleo yoyote.

Katika zoezi la kukusanyajiwa fedha hizo vitongoji vya Mlafu na isagwa vilikamilisha michango hiyo ila kitongoji cha Itungi hakikuweza kukamilisha michango hiyo.

Aidha, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Itungi Nerdy Kasian Kipemba (Chadema) alikanusha tuhuma hizo na kudai kwamba uongozi uliopita ndio ulikuwa na matatizo hayo ya kutokusanya michango hiyo kikamilifu.

Kitongoji cha Itungu ambacho kipo Kata ya Mlafu katika mamlaka ya mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo, kinaongozwa na Chama cha Chadema.

Kitongoji hicho kwa sasa kinaongozwa na kaimu mwenyekiti Elia Luka Mposewa mpaka hayo utaratibu wa kumpata mwenyekiti mpya utakapoandaliwa.

Awali, Afisa Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Ilula Edward Mbembe akisoma taarifa mbele ya Mkuuwa Wilayaya Kilolo Asia Abdallah kuwa kutokana na kitongoji cha Itungi kutokamilisha michango hali hiyo wananchni wa vitongoji vya Isagwa na Mlafu nao waliamua kurudi nyuma katika uchanganyaji wa shughuli za maendeleo ya kata.

Alisema kuwa uongozi wa mamlaka ya mji mdogo wa Ilula na tarafa ya Mazombe ulifika katika kitongoji cha Itungi na kufanya vikao vya ndani na baadae mkutano wa hadhara.

Makubaliano yalifikikwa kwa wananchi ni kuwa mwenyekiti wa kitongoji atoe ushirikiano katika kusanya michango ili shughuli za maendeleo zisikwame.

Mbembe alisema kuwa hali hiyo ya kutotoa ushirikiano katika ukusnayaji michango iliendelea ambapo mtendaji wa kata ya mlafu alimshitaka mwenyekiti wa kitongoji cha Itungi mahakamani na mwisho wa kesi hiyo iliamuru kwenda kukusanya michango hiyo.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...