Skip to main content

DKT ANGELINE LUTAMBI AZINDUA “IKUNGI ELIMU CUP 2017” AMFAGILIA DC MTATURU KWA UBUNIFU










Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi akihutubia mamia ya wananchi wa Wilaya ya Ikungi waliojitokeza katika hafla ya uzinduzi wa Mashindano ya Mpira wa miguu ya “IKUNGI ELIMU CUP 2017”



Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi akihutubia mamia ya wananchi wa Wilaya ya Ikungi waliojitokeza katika hafla ya uzinduzi wa Mashindano ya Mpira wa miguu ya “IKUNGI ELIMU CUP 2017”


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisoma taarifa ya “IKUNGI ELIMU CUP 2017” mbele ya Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi wakati wa ufunguzi wa mashindano ya mpira wa Miguu.



Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akibeba tofali lililofyatuliwa na Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi wakati wa ufunguzi wa mashindano ya mpira wa Miguu ya “IKUNGI ELIMU CUP 2017”



Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Singida Ndg Jimson Mhagama akibeba tofali lililofyatuliwa wakati wa ufunguzi wa zoezi la ufyatuaji matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara na madarasa.



Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akifyatua matofali wakati wa ufunguzi wa zoezi la ufyatuaji matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara na madarasa.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Ikungi akifyatua matofali wakati wa ufunguzi wa zoezi la ufyatuaji matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara na madarasa.



Kikosi cha Timu ya Ikungi United 



Kikosi cha Timu ya Puma Combine kilichoshinda goli 3 kwa 2 dhidi ya Ikungi United 



Moja ya wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita kwa kupata Daraja la kwanza akipokea shilingi 100,000 ikiwa ni ahadi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji J. Mtaturu 



Matofali ambayo yamefyatuliwa na wadau wakati wa ufunguzi wa ufyatuaji matofali Wilayani Ikungi 








Mipira iliyotolewa kwa jili ya timu zote washiriki wa “Ikungi Elimu Cup 2017”








Na Mathias Canal, Singida




SERIKALI imekuwa ikifanya jitihada za dhati katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, Nyumba za walimu, Maabara, Matundu ya vyoo na mabweni.






Ili kunusuru kadhia hiyo imeelezwa kuwa moja ya mikakati ni pamoja na wakuu wa Wilaya kuwashirikisha wananchi pamoja na wadau wa elimu kuchukua hatua madhubuti ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto na hatimaye kuwafanya wanafunzi wawe na furaha na amani. 






Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Wilaya ya Ikungi waliojitokeza katika hafla ya uzinduzi wa Mashindano ya Mpira wa miguu yanayojulikana kama “IKUNGI ELIMU CUP 2017” itakayofanyika katika vijiji vyote 101 vilivyopo katika wilaya ya Ikungi.






Mashindano hayo yaliyoanza leo Agosti 19, 2017 katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Ikungi yanataraji kufika ukomo siku ya Jumanne Septemba 19, 2017 kwa matazamio ya kuwafikia zaidi ya wanachi 5000 katika Wilaya hiyo.






Dkt Lutambi alisema kuwa Mashindano hayo yenye kauli mbiu isemayo “CHANGIA, BORESHA ELIMU IKUNGI” yamebeba mtazamo chanya wa elimu wenye manufaa kwa wananchi katika kizazi cha sasa kuelimika na kizazi kijacho.






Alitumia nafasi hiyo pia kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu huku akiwaeleza wananchi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli alichagua mtu muhimu kumuwakilisha katika Wilaya hiyo kwani ubunifu wake katika utendaji una manufaa makubwa kwa wananchi na jamii kwa ujumla.






Awali akisoma taarifa ya uzinduzi wa Mashindano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa mashindano hayo ambayo yatakuwa yanalenga kuhamasisha wananchi na wadau mbalimbali kuchangia vitu mbalimbali kwa ajili ya kuboresha changamoto zinazoikabili sekta ya elimu katika Wilaya ya Ikungi ikiwemo upungufu wa nyumba za walimu, maabara ya masomo ya sayansi kwa shule za sekondari, Madarasa kwa shule za msingi pamoja na vifaa vya kujifunzia.






Sambamba na mashindano hayo ya mpira wa miguu lakini pia umezinduliwa ufyatuaji wa matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya masomo ya Sayansi ambazo zipo katika hatua za msingi kwa muda mrefu.






Aidha, zimetolewa zawadi kwa wanafunzi waliopata daraja la kwanza (Division One) katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka huu 2017 na walimu wao ikiwa ni ahadi iliytolwa na mkuu wa wilaya hiyo.






Mhe Mtaturu aliahidi kutoa shilingi laki moja kwa kila mwanafunzi atakayepata Daraja la Kwanza na shilingi milioni moja kwa walimu kwa wanafunzi 10 watakaopata Daraja la Kwanza.





MWISHO Na Mathias Canal, Singida 




SERIKALI imekuwa ikifanya jitihada za dhati katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, Nyumba za walimu, Maabara, Matundu ya vyoo na mabweni.






Ili kunusuru kadhia hiyo imeelezwa kuwa moja ya mikakati ni pamoja na wakuu wa Wilaya kuwashirikisha wananchi pamoja na wadau wa elimu kuchukua hatua madhubuti ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto na hatimaye kuwafanya wanafunzi wawe na furaha na amani. 






Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angeline Lutambi wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Wilaya ya Ikungi waliojitokeza katika hafla ya uzinduzi wa Mashindano ya Mpira wa miguu yanayojulikana kama “IKUNGI ELIMU CUP 2017” itakayofanyika katika vijiji vyote 101 vilivyopo katika wilaya ya Ikungi.






Mashindano hayo yaliyoanza leo Agosti 19, 2017 katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Ikungi yanataraji kufika ukomo siku ya Jumanne Septemba 19, 2017 kwa matazamio ya kuwafikia zaidi ya wanachi 5000 katika Wilaya hiyo.






Dkt Lutambi alisema kuwa Mashindano hayo yenye kauli mbiu isemayo “CHANGIA, BORESHA ELIMU IKUNGI” yamebeba mtazamo chanya wa elimu wenye manufaa kwa wananchi katika kizazi cha sasa kuelimika na kizazi kijacho.






Alitumia nafasi hiyo pia kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu huku akiwaeleza wananchi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli alichagua mtu muhimu kumuwakilisha katika Wilaya hiyo kwani ubunifu wake katika utendaji una manufaa makubwa kwa wananchi na jamii kwa ujumla.






Awali akisoma taarifa ya uzinduzi wa Mashindano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa mashindano hayo ambayo yatakuwa yanalenga kuhamasisha wananchi na wadau mbalimbali kuchangia vitu mbalimbali kwa ajili ya kuboresha changamoto zinazoikabili sekta ya elimu katika Wilaya ya Ikungi ikiwemo upungufu wa nyumba za walimu, maabara ya masomo ya sayansi kwa shule za sekondari, Madarasa kwa shule za msingi pamoja na vifaa vya kujifunzia.






Sambamba na mashindano hayo ya mpira wa miguu lakini pia umezinduliwa ufyatuaji wa matofali kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya masomo ya Sayansi ambazo zipo katika hatua za msingi kwa muda mrefu.






Aidha, zimetolewa zawadi kwa wanafunzi waliopata daraja la kwanza (Division One) katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka huu 2017 na walimu wao ikiwa ni ahadi iliytolwa na mkuu wa wilaya hiyo.






Mhe Mtaturu aliahidi kutoa shilingi laki moja kwa kila mwanafunzi atakayepata Daraja la Kwanza na shilingi milioni moja kwa walimu kwa wanafunzi 10 watakaopata Daraja la Kwanza.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...