Skip to main content

HAKIARDHI KUPIMA MASHAMBA 900 WILAYANI KILOLO


Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (HAKIARDHI) na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa wakitialiana saini mkataba wa makubaliano ya mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji (VLUP) Ijumaa wilki iliyopita ambapo mashamba 900 katika vijiji vya Lukani, Ng’ang’ange na Mdeke wilayani humo vitapitiwa na mpango huo. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Ernest Upemba, Mweneyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Venance Kiwhanga, Afisa Programu wa HAKIARDHI Cathbert Tomitho na Mwanasheria wa Taasisi ya HAKIARDHI Joseph Chiombola. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)


Na Friday Simbaya, Kilolo

Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (HAKIARDHI) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa imepanga kupima mashamba 900 katika vijiji vitatu wilayani kupitia mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji (VLUP).

Katika mpango huo HAKIARDHI imepanga kupima vipande vya ardhi na mashamba 900 katika vijiji vitatu vya Lukani, Ng’ang’ange na Mdeke ambapo kila kijiji kitapimiwa mashamba 300 kupitia Programu ya Ardhi Yetu (AYP) kwa ufadhaili wa shirika la CARE International Tanzania.

Makabaliano hayo walitiwasaini Ijumaa wiki iliyopita na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Ernest Upemba kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo na Afisa Programu wa HAKIARDHI Cathbert Tomitho kwa upande wa HAKIARDHI.

Makataba wa makubaliano ulishuhudia na Mweneyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Venance Kiwhanga kwa upande wa halmashauri ya kilolo na Mwanasheria wa Taasisi ya HAKIARDHI Joseph Chiombola.

Awali, Chiombola alisema kwa Mradi Mpya Wa Vijiji Vitatu umepanga kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi kwenye vijiji vipya 3, ambao utagharimu jumla ya shilingi milioni themanini na saba nukta nne (87.4m/-), hivyo kufanya jumla ya vijiji vilivyosapotiwa na HAKIARDHI kuwa 16. 

Vijiji hivyo ni Kihesamgagao, Kiwalamo, Kidabaga, Kipaduka, Ibofwe, Kitelewasi, Uhambingeto, Ilamba, Lugalo, Lyamko, Itonya na Vijiji vipya ni Ng’ang’ange, Mdeke na Lukani, Tayari utafiti wa awali wa kubainisha mahitaji ulishafanyika mwezi Julai 2017,

Alisema kuwa Matokeo ya utafiti yanaonesha vijiji hivyo vina changamoto kwa mfano, migogoro ya ardhi, hatari ya uhaba wa chakula, ukiukwaji haki za wanawake katika umiliki wa ardhi, na adhari ya mabadiliko ya tabianchi kupitia program ya ardhi yetu (AYP).

Chiombola alisema AYP ina malengo yafuatao; Kukuza uelewa wa wananchi juu ya masuala ya ardhi na ushiriki wao katika maamuzi yanayohusu ardhi na rasilimali vijijini, Kuimarisha vyombo vya utoaji maamuzi na haki juu ya ardhi katika serikali za mitaa (H/Kijiji, M/Kijiji).

Kuimarisha mikakati ya wananchi na viongozi wa serikali za mitaa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na Kuimarisha uwajibikaji wa serikali za mitaa kwa wananchi.

Naye mwakilishi kutoka tume ya taifa ya mipnago ya matumzi ya ardhi (NLUPC) Experancia Tibasama ametoa wito kwa halmashauri hiyo kuandaa wananchi hasa katika vijiji vinavyo husuka na mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji iliwaweze kushiriki kikamilifu.

Kwa upande wake Mweneyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Venance Kiwhanga aliishukuru taasisi ya hakiardhi na wadau wengine wanaoshirikiana na taasisi hiyo kwa kuiwezesha halmashauri kupiga hatua katika utekelezaji wa sheria za ardhi na sheria za utatuzi wa migogoro.

Alisema kuwa halmashauri imeweza kuandaa hatimiliki zaidi ya 6700, kufundisha sheria ya ardhi ya vijiji Na.5 ya mwaka 1999 na sheria ya utatuzi wa migogoro ya mwaka 2002 kwa vijiji vyote.

Pia kupitia shughuli hizo ardhi wameshuhudia mwamko mkubwa wa wananchi hususani katika umilikaji wa ardhi, utawala na utatuzi wa migogoro.

“Tunafarijika sana kuona tunafanya uzinduzi wa mradi mwingine wa vijiji vitatu ambapo inatarajiwa kupima mashamba takribani 900, hakika tunawashukuru sana wadau wote…,” alisema Kiwhanga.

Alisema kuwa pamoja na mchango wa wadau mbalimbali kwenye masuala ya ardhi katika Wilaya ya Kilolo, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazogusa jamii kama vile; mitazamo ya kijamii juu ya haki ya mwanamke kumiliki ardhi, uuzaji holela wa ardhi kwa baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Kilolo.

Hata hivyo, halmashauri ya wilaya ya kilolo, mkoani iringa inajumla ya vijiji 94 lakini vijiji 40 tu ambavyo vina mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji kwa mujibu wa afisa ardhi wa wilaya ya kilolo, Elinaza Kiswaga.

Mwisho







Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...