Skip to main content

MAGHEMBE AFUTA MIKATABA YA UWINDAJI, AVUNJA BODI YA MBOMIPA


















WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe ameivunja bodi ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Tarafa ya Idodi na Pawaga (Mbomipa) pamoja na kufuta mikataba ya kampuni mbili zinazoendesha shughuli za uwindaji wa kitalii katika eneo hilo.


Mbomipa ni eneo la hifadhi ya jamii ya wanyamapori linalopakana na hifadhi ya Taifa ya Ruaha, wilayani Iringa mkoani Iringa lenye wanyamapori wengi wanaoingia na kutoka katika hifadhi hiyo linaloundwa na vijiji 21 vya tarafa hizo mbili.


Bodi iliyovunjwa inaundwa na Mwenyekiti Zabron Luvinga na Steven Nyandongo, Alban Lutambi, Mawazo Malembeka na Denis Ngede ambao ni wajumbe; na kampuni zilizofutiwa mikataba ni Kilombero North Safaris Ltd na Mkwawa Hunting Safaris Ltd.


Wakati mmiliki wa kampuni ya Mkwawa Hunting Safaris Ltd Ahamed Huwel alisema amepokea bila kinyongo chochote uamuzi huo wa waziri alioutangaza juzi mbele ya wanajumuiya hiyo katika kijiji cha Tungamalenga, mmiliki wa Kilombero North Safaris Ltd, Acram Aziz hakupatikana kuzungumzia uamuzi huo.


Hatua ya Waziri Maghembe kuvunja bodi na kufuta mikataba ya jumuiya hiyo na kampuni hizo imekuja kwa kuzingatia matokeo ya timu ya wataalamu aliyoiunda hivikaribuni kuchunguza dosari na malalamiko ya uendeshaji wa taasisi hiyo na kubaini mapungufu makubwa ya kisheria na kiutendaji.


“Kwanza Katiba inayotumiwa na jumuiya hii inakinzana na sheria za wanyamapori, kanuni za uwindaji wa wanyamapori na utalii wa kupiga picha; lakini pia bodi haiko pamoja, kila upande una mwekezaji wake,” alisema.


Kwa mazingira hayo, waziri huyo alisema katiba ya jumuiya hiyo inatakiwa kufumuliwa upya na baada ya hapo bodi mpya uindwe katika mchakato alioagiza uwe umakamilika kabla ya Oktoba mwaka huu na baada ya hapo shughuli ya kutafuta wawekezaji ianze upya.


Profesa Maghembe alisema eneo la jumuiya hiyo lina utajiri mkubwa lakini akashangaa kuambiwa kwamba wana jumuiya hawana wanachopata kutokana na uwekezaji unaofanywa eneo hilo, jumuiya haina uwezo wa kulipa mishahara watumishi na walinzi wake na inashindwa kufanya shughuli zake mbalimbali za kiofisi na matengenezo ya vifaa na gari lao yamekuwa yakifanywa kwa kupitisha bakuri.


Awali katibu wa Mbomipa, Josephat Kisanyagi alisema jumuiya imekuwa katika mtikisiko mkubwa wa kukosa mapato kutoka kwa wawekezaji wake katika kipindi chaJulai 2016 hadi sasa.


“Kukosekana kwa mapato hayo kumesimamisha shughuli muhimu za jumuiya hiyo huku viongozi na walinzi wanaofanya kazi ya doria katika eneo hilo la Mbomipa wakikosa mishahara na stahiki zao,” alisema.


Akionekara kukerwa na kile kinachoendelea ndani ya jumuiya hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema; “hakuna kijiji hata kimoja kati ya vijiji 21 vinavyounda jumuiya hiyo kinachoweza kusema kimenufaika na uwepo wa Mbomipa.”


Masenza alisema katika jumuiya hiyo pamekuwepo na migongano isiyokwisha na utapeli uliokithiri ambao sehemu yake kubwa ulifanywa na bodi zilizopita kana kwamba Mbomipa ilikuwa mali yao.


“Kwa maneno mepesi bodi ilipewa mamlaka na madaraka makubwa juu ya Mbomipa kuliko inavyotakiwa, kumekuwa na kufukuzana na kuchaguana mara kwa mara kwasababu baadhi ya watu waliokuwa wakipata uongozi waliomba uongozi ili kukidhi maslai yao,” alisema.


Akiahidi kuyasimamia maamuzi hayo ya waziri, Masenza aliwageukia pia baadhi ya wawekezaji katika eneo hilo la Mbomipa akisema wamekuwa matapeli na hivyo kuifanya jumuiya hiyo ifike hapo ilipo na kugeuka kuwa ombaomba.


Baada ya taarifa hiyo ya mkuu wa mkoa, Profesa Maghembe aliiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi wa mapato na matumizi ya jumuiya hiyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa watu watakaobainika waliitumia kujinufaisha.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...