Skip to main content

WAUZA MAGAZETI MKOANI IRINGA WAIOMBA JAMII KUTHAMINI KAZI YAO


WAUZA magazeti mkoani Iringa wameiomba jamii kuthamini kazi yao ya kuuza magazeti na kuachana na dhana potofu ya kuwaona kama ni watu wasiofaa katika jamii.

Wauza mgazeti hao waselima hayo wakati wakiongea na Nipashe jana kupitia umoja wa wauuza magazeti Iringa (UWAMAI), nakuongeza kuwa wameamua kuanziasha umoja huo ili kuondoa dhana potofu ya jamii juu yao.

Walisema kuwa wapo watu wanaowafananisha na wahuni, wavuta bangi na wasiokuwa na maadili katika jamii na wengine kuwahisi kuwa na itikadi Fulani wa vyama vya siasa.

Akifafanua kuhusu jambo hilo mweneyekiti wa umoja huo wa UWAMAI, Mashaka Kayoka alisema kuwa kazi ya kuuza magazeti ni kazi kama kazi zingine za kujiingizia kipato.

Kayoka aliwaomba wadau mbalimbali wa magazeti pamoja na serikali kuviunga mkono vikundi kama hivyo kwa kuthamini kazi zao yakusambaza magazeti kwa wateji mbalimbali ili wapate habari.

“Tumekuwa tukinyoshewaa vidole na jamii kwamba wauza magazeti ni wahuni na watu wa vurugu, kumbe wala sisi tunafanyakazi yetu yakutuingizia kipato. Sisi pia tuna familia na tunatunza familia zetu kupitia kazi hii pamoja na kusomesha watoto wet shule…,” alisema Kayoka.

Alisema kuwa lengo la kuunda umoja huo ni kusaidiana katika shida na raha akatoa mfano kuwa , mwanachama akiugua au akiunguliwa, akifiwa au akifa umoja huo unamsaidia kwa kutoa kidogo fedha katika kafanikisha matibabu au mazishi.

Naye Katibu wa UWAMAI, Bernard Makoli alisema kuwa umoja wao umesajiliwa rasmi na mamalaka husika na kupewa namba ya usajili IR/IMC/CBO NO.208 na kuruhusiwa kufanya shughuli zake katika Manispaa ya Iringa, na kwa mkoa wa Iringa kwa ujumla.

Makoli aliwaomba wadau wa magazeti pamoja na makampuni mbalimbali ya magazeti kuwaunga mkono katika shughuli zao za kila siku.

“Tunafanya kazi ya kusambaza habari kupitia kuuza magazeti kwa hiyo wenye magazeti waone umuhimu ya kuwasaidia na kuwezesha kwa hali na mali…,” alisema.

Aliongeza kuwa umoja huo pia ufanyakazi ya kuelimisha jamii ili iondokane na umasikini kwa kuhamasisha jamii kupitia kazi zao za vikundi ili kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo.

Kwa upande wake mweka hazina wa umoja huo Salum Hamisi alisema kuwa kikundi chao kinapata mapato kupitia ada na michango mbalimbali za wanachama.

Alisema kuwa wanaomba taasisi za kibenki na wadau mbalimbali kuwaunga mkono jitihada zao kwa kuwawezesha ili waweza kutunisha mfuko ili wawezi kukopeshana na hatimaye kujikwamua katika umasikini wa kipato.

Na Friday Simbaya, Iringa





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...