Skip to main content

MAJALIWA MGENI RASMI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya utalii yajukalikanayo kama Karibu Kusini-Tanzania Southern Circuit yanataraijiwa kufanyika kwenye viwanja vya Kichangani, Iringa mjini, mkoani Iringa, kuanzia tarehe 27.09.2017 hadi 02.10.2017 jana. (Picha na Friday Simbaya)




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maonesho ya utalii yajukalikanayo kama Karibu Kusini-Tanzania Southern Circuit yanataraijiwa kufanyika kwenye viwanja vya Kichangani, Iringa mjini, mkoani Iringa, yatakayofunguliwa tarehe 29.09.2017.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (Jumatatu) Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema maonesho hayo yataanza tarehe 27 Septemba hadi 02 Oktoba, 2017.

Alisema kuwa mikoa ya nyanda za juu kusini (iringa, njombe, mbeya, songwe na ruvuma) kwa kushirikiana na wizari ya maliasili na utalii, shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) pamoja na wadau mbalimbali wanaandaa maonesho.

Masenza alisema kuwa mwaka 2009, mkoa wa iringa uliteuliwa na wizara ya maliasilina utalii kuwa kitovu cha utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini.

Alisema kuwa kutokana na uteuzi huo, mkoa wa iringa umepata heshima ya kuaandaa maonesho hayo.

“Lengo kuu ni kutangaza fursa na vivutio vya utalii vilivyopo katika mikoa ya nyanda za juu kusini ili wananchi na wageni kutoka ndani na nje wavifahamu na kuvitembelea na hivyo kukuza utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini,” alisema masenza.

Alivitaja vivutio vilivyopo katika nyanda za juu kusini kama vile vya kihistoria, kiutamaduni na kiikolojia ambavyo vinafanya upekee wa mikoa hiyo katka utalii.

Maonesho ya utalii karibu kusini yanakwenda sambamba na maandhimisho ya kitaifa ya siku ya utalii duniani mwaka 2017 ikijumuisha pia maoneshoya bidhaa za wajasiriamali kutoka katika mikoa ya nyanda za juu kusini na mikoa minigine ya Tanzania.

Kwa mwaka huu 2017 maadhimisho ya siku ya utalii yanaongozwa na kauli mbiu isemayo, “ UTALII NI NGUZO YA UCHUMI WA VIWANDA.”

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...