Skip to main content

MSIGWA AACHIWA KWA DHAMANA BAADA YA KUHOJIWA MASAA SITA NA POLISI



Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo (Jumatatu) akizungumzia suala la kushushwa jukwaani kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Mlandege mkoani Iringa kukamatwa na polisi jumapili. 


IRINGA: Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) pichani amesema kutendo cha polisi kushushwa jukwaani kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya mlandege mjini Iringa jana kimemudhalilisha kama kiongozi wa kuchaguliwa na wananchi.

Mchungaji Msigwa ambaye yupo nje kwa dhamana alisema hayo (jumatatu) katika mkutano na waandishi wa habari ofisin kwake nakuongeza polisi wamevunja sheria ya bunge yaani, sheria ya Parliamentary Immunity Powers and Privileges Act of 1988 kwa kuvuruga mkuatano wake.

Alisema kuwa sheria hiyo inampa mamlaka ya kutimiza wajibu wake kama mbunge wakati akiongea na wananchi.

Mbunge huyo alikamatwa na polisi Jumapili jioni baada ya kushushwa jukwaani kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Mlandege mkoani Iringa kwa kudai kwamba ametoa maneno ya uchochezi.

Alisema kuwa Hali ya kukamatwa kamatwa ya Wabunge wa Upinzani Nchini Hususani Chadema ilikuwa imetulia baada macho na masikio ya wengi kuelekezwa kwenye kumtibu Mbunge wa Singida masharki ,Tundu Lissu ambaye alipigwa risasi na watu wasiojulikana mwanzoni mwa mwezi huu mjini Dodoma.

Hali ya kukamatwa kamatwa ni kama imeanza tena ndivyo naweza kusema baada,Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa (Chadema) kukamatwa na polisi leo Jumapili jioni baada ya kushushwa jukwaani kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Mlandege mkoani Iringa.

Mchungaji Msigwa alisema kuwa anakusudia kumfungulia mashitaka Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya (OCD) kwa alichodai kwamba alitumia madaraka vibaya.

“Nipo mbioni kumpeleka mahakamani OCD kwa kutendo cha kunishua jukwaani na kunikamata wakati natimiza majukumu yangu kibunge pamoja na kuvunja sheria ya sheria ya Parliamentary Immunity Powers and Privileges Act of 1988,” alisema Msigwa.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema Iringa Mjini (Bavicha), Leonce Marto alisema kuwa mbunge huyo alikamatwa saa 11:24 jioni na Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (RCO) aliyekuwa ameambatana na polisi wengine kisha wakampeleka ofisi za mkoa za jeshi hilo.

“Kutoka Mlandege mpaka ofisini kwa kamanda wa mkoa amebadilishwa kwenye magari matatu. Tunahisi atakuwa anasafirishwa ingawa bado anahojiwa. Yupo ndani, sisi tunaendelea kumsubiri nje,” alisema Marto.

Mwenyekiti alibainisha kwamba mpaka wakati huo (saa 12:30 jioni) jeshi hilo halikubainisha sababu za kumshikilia Msigwa.

“Alikuwa na kibali cha kufanya mkutano katika kata tatu kuanzia leo Jumapili mpaka Jumanne. Alianza kuzungumza saa tisa alasiri ilipofika saa 11:24 jioni,RCO akiwa na polisi wengi wakamshusha jukwaani na kuondoka naye,” alisema Marto bila kufafanua sababu za kukamatwa.


Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa (RPC) Julius Mjengi alithibitisha kukamwata kwa mbunge wa iringa mjini nakuongeza kuwa alikamatwa kwa kutoa lugha ya uchocheza kwa kuchonganisha jeshi la polisi na wananchi.

RPC alisema kuwa Mchungaji Peter Msigwa yupo nje kwa dhamana baada ya kuhojiwa kwa masaa sita.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...