Skip to main content

TANAPA: INAKUPELEKA KUTALII HIFADHI YA RUAHA KWA 30,000/- TU KWENDA NA KURUDI




IRINGA: Wananchi wa mikoa ya nyanda za juu kusini wameaswa kutumia fursa ya siku mbili maonesho ya utalii karibu kusini kuitembelea hifadhi ya taifa ya Ruaha iliyopo wilayani Iringa, mkoani Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari ya meneja masoko wa shirika la hifadhi za Tanzania (TANAPA) aliwaomba wananchi kutumia siku mbili za maonesho ya utalii yanayofanyika kwa wiki moja mjini iringa kwenda hifadhi ya ruaha kwa gharama nafuu.

Alisema kuwa TANAPA kupitia maonesho ya utalii ya karibu kusini inatenga siku mbili maalumu kwa ajili wananchi kwa ajili ya wananchi kutembelea hifadhi hiyo kwa gharama nafuu katika ya septemba 28 -30 mwaka huu.

“Kwa kupitia ofa hiyo kutakuwa na mchango mdogo wa fedha; mtu mzima atalazimika kuchangia Sh 30,000 na mtoto Sh 10,000 tu kumuwezesha kwenda kwa siku moja kutalii katika hifadhi hiyo kubwa kuliko zote nchini,” alisema.

Alisema mchango huo unahusisha gharama ya usafiri, kiingilio cha hifadhini, utalii na muongoza wageni atakayewapitisha katika vivutio mbalimbali ndani ya hifadhi hiyo.

“Tuna nafasi 50 tu tumetoa kwa kupitia ofa hii. Safari ya kwanza itahusisha watu 25 na safari ya pili watu 25 pia, kwahiyo wanaotaka wafike na kujiandikisha katika banda letu lililopo katika viwanja vya Kichangani yanapofanyika maonesho haya,” alisema.

Akizungumzia baadhi ya vivutio vilivyoko katika hifadhi hiyo, Mhifadhi wa Idara ya Utalii Ruaha, Hellen Mchaki alisema Hifadhi ya Ruaha pamoja na wingi wa vivutio inabeba pia historia muhimu ya Chifu Mkwawa, kiongozi wa kabila la Wahehe mkoani Iringa aliyeongoza mapambano dhidi ya wajerumani katika karne ya 19.

Alitaja baadhi ya wanyama waliopo katika hifadhi hiyo kuwa ni kudu wakubwa na wadogo, viboko, mamba, pofu, swala pala, makundi makubwa ya samba, tembo na nyati, chui, mbweha, fisi, twiga, pundamilia na mbwa mwitu.

Akizungumzia idadi ya watalii katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, Mchaki alisema mwaka 2012/2013 walipokea watalii wa nje 14,299 na wa ndani 9,094, mwaka 2013/2014 wa nje 13,489 na wa ndani 9,673 na mwaka 2014/2015 wa nje 13,272 na wa ndani 8,291.







Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...