Skip to main content

WANAFUNZI NA WALIMU WA SHULE YA UFUNDI IFUNDA WAMPONGEZA JPM KWA UKARABATI


makamu mkuu wa shule Peter Mbata (kulia) na Amon Chota (mtaaluma).


mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya ufundi Ifunda, Mpambwe Paul 



mafundi wakiendelea na ukarabati wa shule kongwe ya ifunda ufundi kama walivyokutwa na mwandishi wetu jana (Picha na Friday Simbaya)




Wanafunzi na walimu wa shule ya ufundi Ifunda (Ifunda Technical Secondary School) mkoani iringa wameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufufua na kuboresha miundombinu ya shule yao.

Walisema kuwa baada ya mpango wa serikili kuamua kuanza ukarabati wa shule kongwe nchini ikiwemo Ifunda utachangia ufaulu bora kwa wanafunzi pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kufundishia na kujisomea.

SIMBAYABLOG jana ilitembea shule hiyo kongwe ya Ifunda na kujionea ukarabati unaondelea kwa kusimamiwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya (MUST). 

Derika Makoi ni mwanafunzi wa kidato cha tatu alibainisha kuwa ukarabati huo unaoendelea utachangia wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao kwani hapo awali wakati miundombinu ilikuwa mibaya wanafunzi walikuwa wanatumia mishumaa kujisomea.

Alisema kuwa ukabarati ambao unaendelea katika madarasa na mabweni umeboresha mazingira ya wanafunzi ya kujisomea kwani hata madarasani kumekuwa na umeme wakati hapo awali wanafunfuzi walikuwa nasomea mabwenini.

Makoi alisema kujisomea mabwenini hakukuwa rafiki sana kwa kujisomea kwani kulikuwa na mchanganyiko wa wanafunzi wanaolala humo na pengine makelele kutoka kwa wanafunzi wa madarasa ya chini.

“Tulikuwa tunalazimika kutumia mishumaa kujisomea madarasani kwa vile madarasa hayakuwa na umeme lakini kwa sasa tunashukuru serikali kwa kukarabati pamoja na kuboresha miundombinu ya shule yetu,” alisema Makoi.

Alisema kuwa katika ukarabati unaoendelea umekuwa na faida nyingi kuliko hasara kwa wanafunzi sasa wanajiamini kwa kujisomea muda wote kwa sababu madarasani kuna mwanga muda wote.

Mwanafunzi mwingine wa kidato cha tatu alisema ukarabati huo umeboresha mazingira katika madarasa kwa madarasa mengi hayakuwa na milango na vioo madirishani kipindi cha baridi walikuwa wanapata shida.

Alisema kuwa kuna wakati mwingine upepo ulikuwa unapuliza mpaka kupeperusha makaratasi wakati wa kujisomea lakini baada ya ukarabati mazingira yamekuwa mazuri.

Alisema hapo awali madarasa machache yalikuwa na umeme kwa hiyo wanafunzi wanafanya prepo muda wote kutokana na madarasa mengi kuwa na umeme mpaka wanajisomea hadi usiku.

Alisema kuwa ukarabati pia uangalie suala la maji kwani shule hiyo ina miundmbinu mibovu ya maji kwani wanafunzi wanatumia muda mwingi kutafuta maji kutokana na visima vya maji kuwa vichache.

Alisema kuwa maji ni afya kwa hiyo serikali isaidie pia katika kuboresha miundombinu ya maji shuleni ili wanafunzi watumie muda mwingi kujisomea.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya ufundi Ifunda, Mpambwe Paul aliishukuru serikali kwa kukarabati shule yao kwani mpango utainua kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.

Alisema kuwa kupitia mpango huo mazingira ya shule pia utachangia ufaulu bora kwa wanafunzi na pia watakuwa na mazingira bora ya kufundishia kwa vile miundombinu itakuwa rafiki kwa kufundishia na kujisomea kwa upande wa wanafunzi.

Walimu wengine waliounga mkono mpango wa serikali kwa ukarabati huo ni makamu mkuu wa shule Peter Mbata na Amon Chota (mtaaluma).

Mpambwe alisema kuwa ukarabati huo unahusisha madarasa yote, mabweni yote pamoja na jengo la utawala isipokuwa nyumba za walimu.

Hivi karibuni serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi, teknolojia na mafunzo imeanza mpango kabambe wa kukarabati shule zote kongwe nchini baada ya shule kongwe za Serikali kufanya vibaya katika mitihani ya taifa kwa kipindi cha takribani miaka mitano mfululizo.

Serikali imeanzisha mpango kabambe wa kufufua hadhi na kuziboresha zaidi shule hizo.

Katika Bunge lililopita, Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Dk Joyce Ndalichako alibainisha kuwa kwenye bajeti ya mwaka 2016/17, Serikali imetenga jumla ya Sh bilioni 33 kwa ajili ya kukarabati shule kongwe zote nchini na kwa kuanza, jumla ya shule 20 zitakarabatiwa kupitia mpango huo ambapo Sh bilioni 20 zimetengwa kwa kazi hiyo.

Ilisema kuwa shule kongwe 10 Jangwani, Azania, Kibaha, Nangwa, Kigoma, Tosamaganga, Shule ya Wasichana ya Songea, Malangali, Mirambo na Minaki tayari zimekabidhiwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na kazi ya ukarabati imeanza na zinatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu.

Shule 10 nyingine ambazo ni Mpwapwa, Kibiti, Ifakara, Bwiru -Wavulana, Kantalamba, Moshi-Ufundi, Tanga-Ufundi, Musoma- Ufundi, Ifunda - Ufundi na Mtwara- Ufundi zimekabidhiwa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya (MUST).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...