Skip to main content

WANANCHI WANAOTAKIWA KUPISHA MRADI WA SHANTA GOLD MINE WILAYANI IKUNGI MALIPO YAO


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.


Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.


Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu akielezea utaratibu wa ulipaji fidia kwa wanufaika.


Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na wananchi mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.


Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd. 


Na Mathias Canal, Singida

Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida huenda ikaanza uchimbaji wa madini ya dhahabu hivi karibuni baada ya kuanza kulipa fidia ya zaidi ya Bilioni 1.6 wanufaika wa awamu ya pili inayohusisha wananchi kutoka Vijiji vitatu vya Mang'onyi, Sambaru na Mulumbi.


Kampuni hiyo tayari imekamilisha ulipaji wa awamu ya kwanza kwa kulipa zaidi ya Milioni 900.2 Wanufaika waliolipwa fedha hizo wanaotokana na mazoezi mawili ya uthamini yaliyofanywa kwenye eneo la mradi kwa ajili ya upanuzi wa kambi.


Malipo hayo yatakamilisha umiliki wa maeneo hayo kwa Kampuni ya Shanta Gold mining kwa ajili ya uchimbaji na kuwafanya wananchi hao kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu pasina kinyongo chochote.


Malipo hayo ya awamu ya pili na ile ya kwanza yamelipwa kwa wanufaika wote wa fidia katika Vijiji vyote vilivyopo Katika Kata ya Mang'onyi yanaondoa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa maeneo mbalimbali waliopo kwenye eneo la mradi huo waliotaka kufahamu hatima ya malipo yao.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi na wawakilishi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa kampuni hiyo inapaswa kutumia muda mfupi katika ulipaji wa fidia kama ilivyofanya katika awamu ya kwanza.


Alisema kuwa Kampuni hiyo ya uchimbaji imeanza kutekeleza sheria ya madini inayoelekeza miezi sita kabla ya kuanza uchimbaji wawekezaji wanapaswa kuanza kulipa fidia.

Naye Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu alisema kuwa kampuni yake imeanza kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu mwezi Disemba 2016 ya kuwalipa wanufaika hao fidia ambayo ni hatua muhimu ya utekelezaji wa mradi huo.


Alisema kuwa malipo yanafanywa na kampuni hiyo chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya sambamba na wenyeviti wa serikali za vijiji vyote vilivyopo ndani ya mradi.


Kuanza kwa uchimbaji wa madini katika eneo hilo kutaibua ajira nyingi kwa wananchi Wilayani Ikungi na Taifa kwa ujumla jambo litakalosaidia ukuzaji wa pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.



Katika Awamu ya Kwanza Kampuni ya Shanta Gold Mining Ltd iliwalipa wanufaika 92 wenye umiliki wa Viwanja 121 thamani yake ikiwa ni Shilingi 902,412,247.00 Hulu awamu hii ya Pili wakilipwa Wamiliki 114 wenye Viwanja 156 vyenye thamani ya Shilingi 1,663,112,018.01

Aidha, Kuanzia leo Septemba, 2017 wanufaika wa fidia wameanza kufanya uhakiki wa malipo yao na ufunguaji Akaunti kwa ajili ya malipo ikiwa ni matakwa ya kisheria.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mang'onyi Ndg Mohamed H. Ramadhani alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kutoa maagizo ya kulipwa haraka fidia za kila wanufaika Jambo ambalo limetekelezeka kwa haraka katika kipindi Cha muda mfupi.

Sambamba na hayo aliongeza kuwa Mkuu huyo wa Wilaya anafanya kazi kubwa katika kuwaunganisha wananchi wote ili kupata stahiki zao na kufurahia Rasilimali za Nchi yao.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...