Skip to main content

WATAHINIWA 24,906 WA DARASA LA 7 MKOANI WAFANYA MITIHANI



Wakati Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), likitangaza rasmi kuanza kwa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE), kesho Septemba 6 mwaka huu, kote nchini, wito umetolewa kwa wazazi kutobweteka badala yake waanze maandalizi ya watoto hapo baadaye. 

Wito huyo umetolea na Afisa Elimu wa Mkoa wa Iringa (REO) Bw. Majuto Salehe Njanga wakati akiongea na gazeti la mwananchi katika mahojiano maalum leo.

Bw. Njanga alitoa wito kwa wazazi kuwa huu si wakati wa kubweteka na kujisahau na matokeo yake mnashtuka siku za mwisho mtoto ameshachaguliwa kwenda sekondari huku hamjafanya maandalizi.

“Kuanzia sasa wazazi na walezi, anzeni kujiwekea akiba kwa tahadhari ili watoto wenu watakapochaguliwa kuendelea na masomo, basi msione uzito wa kuwapeleka sekondari,” alisema Bw. njanga 
Chonde chonde wazazi wenzangu, endapo mtaanza kujiwekea akiba kidogo kidogo ya kuwapeleka watoto wenu sekondari, ni dhahiri kuwa hamtakosa sare za shule, madaftari na ada, alisema afisa elimu huyo.

Wakati huouhuo, Afisa elimu wa Mkoa wa Iringa Bw. Majuto Salehe Njanga amesema mkoa wa iringa unajumla ya watahiniwa 24,906 ambao watafanya mtihani wa wa kuhtimu elimu ya msingi kwa mwaka 2017.

Alisema kuwa mitihani hiyo itaanza siku ya kesho ya tarehe 6 na itamalizika tarehe 7.

Aliseleza kuwa wasichana wanaotarajiwa kufanya mtihani huo ni 13,412 huku wavulana wakiwa 11,494 kwa shule zote mkoani iringa.

Aidha Bw. Njanga amewataka wanafunzi kuepuka udanganyifu kwa kupewa mitihani nje ya chumba cha mtihani.

Hata hivyo ameongeza kwa kusema kuwa maandalizi yote yameshakamilika kwa shule zote za mkoani wanangoja kesho kuanza mitihani hiyo.

Wataniwa watakaofanya mitihani wa kumaliza elimu ya shule ya msingi kila wilaya ni kama ifuatavyo; manispaa ya iringa ni wanafunzi 3,738 (wasichana 1,976 na wavulana 1,762), wilaya ya iringa ni watahiniwa 6,519 (wasichana 3,493 na wavulana 3,026), Kilolo ni wanafunzi 5,940 (wasichana 3,221 na wavulana 2,719), Mufindi ni 6,820 (wasichana 3,724 na wavulana 3.096) na Mafinga mji ni jumla ya watahiniwa 1,889 (wasichana 998 na wavulana 891). Na Friday Simbaya, Iringa



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...