Skip to main content

WAZIRI LUKUVI ATOA MSAADA WA AMBULANCE JIMBONI KWAKE



Waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi na mbunge wa jimbo la ismani Williamu Lukuvi akiwa kwenye gari la wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser alilokabidhi kwa halmashauri ya wilaya ya Iringa vijijini ambalo ni rafiki na mazingira kwa tarafa ya pawaga mkoani Iringa. 


Waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi na mbunge wa jimbo la ismani Williamu Lukuvi akiwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza sambamba na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela wakitafakari jambo wakati wakukabidhi gari la wagonjwa kwa viongizi wa halmashuri ya wilaya ya Iringa vijijini 


Huu ndio muonekano wa gari la kubebea wagonjwa lililokabidhiwa na waziri Lukuvi kwa ajili ya mahitaji ya kituo cha afya cha Idodi






Waziri wa ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi na mbunge wa jimbo la ismani Williamu Lukuvi ameendelea kuboresha sekta ya afya katika tarafa ya idodi kwa kuwapa gari la kisasa la kubebea wagonjwa linaloendana na mazingira ya tarafa hivyo kwa ajili ya matumizi ya kituo cha afya cha Idodi.


Gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser lilikabidhiwa kwa uongozi wa halmashauri ya Iringa vijijini inayosimamia uendeshaji wa kituo cha afya cha Idodi katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Idodi tarafa ya Idodi.


Akikabidhi msaada huo Lukuvi alisema; “napenda ifahamike kwamba gari hilo limenunuliwa na familia ya Karimjee Jivanjee kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa tarafa ya Idodi na hiyo yote imetokana na uadilifu na uaminifu kwa serilikali ndio umetufanya tushirikiane vyema katika mambo mengi kwa faida ya wananchi wa jimbo langu la Ismani.”

Alisema gari hilo la wagonjwa ni rafiki kwa wagonjwa na wajawazito kwa kuwa lina vifaa tiba vinavyoweza kutumika kutolea huduma wakati wakipelekwa hospitalini.


Baada ya kukabidhi gari hilo, lukuvi ambaye ni mbunge wa jimbo la Ismani, mkoani Iringa alikumbusha vipaumbele vyake kwa wapiga kura wake kuwa ni kuhakikisha jimbo hilo linapata huduma bora ya maji, elimu, afya na miundombinu ya barabara.


MH Lukuvi aliwataka wananchi na viongozi kulitunza gari hilo ili litumike kwa muda mrefu kwa wamanufaa ya wagonjwa.


“Jamani gari hili ni rafiki na mazingira yetu hivyo naombeni tulitunze hili gari kadri tuwezavyo maana magari ya kubebea wagonjwa ni gharama kubwa sana hivyo ni lazima tuwe na uchungu wa vitu tunavyopewa kwa msaada”alisema Lukuvi

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa iringa Amina Masenza alimshukuru waziri Lukuvi kwa kijihada anazozifanya kuboresha sekta ya afya katika jimbo la Ismani.


“Tuna wabunge wengi hapa nchi ila ni wabunge wachache sana ambao wanaokumbuka wananchi wao hivyo niendelee kumpongeza mheshimiwa waziri kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo katika jimbo la Ismani na Iringa kwa ujumla” alisema Masenza 


Akishukuru kwa msaada huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa vijijini, Stephen Mhapa alisema kabla ya msaada huo, kituo hicho cha afya kilikuwa kina gari moja ambalo nalo lilikuwa limeharibia kutokana na kutokuwa na mazingira rafiki na barabara za tarafa hiyo. 

Alisema kupatikana kwa gari hilo jipya kutasaidia kuboresha huduma hiyo kwa kuokoa maisha ya wagonjwa na maisha ya mama na mtoto ambayo ni kipaumbele katika utoaji wa huduma za afya.


Naye diwani wa kata ya Idodi Onesmo Mtatifikolo alisema atahakikisha inatekeleza ahadi mbalimbali zilizotolewa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Dk John Magufuli, mbunge na madiwani ili kuboresha huduma ya afya wananchi wa tarafa ya Idodi.


Nao baadhi ya wanachi wa tarafa ya Idodi walimpongeza waziri Lukuvi kwa msaada wa gari la wagonjwa pamoja na kuanza kutatua tatizo la wafugaji na wakulima kwa vitendo

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...