Skip to main content

KUELEKEA UCHAGUZI MDOGO WA MARUDIO...



Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Ramadhani Kailima. 

WAKATI ikiwa imebakia mwezi mmoja tu kuelekea kwenye uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani kufanyika kutokana na kata mbali mbali kuwa wazi,TUME ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), imesema hati ya kiapo cha mahakama ya kudhibitisha majina ya mtu(Affidavit), haitatumika katika kupiga kura kwenye uchaguzi mdogo wa kata 43.
Hati za kupigia kura zitakazotumika katika uchaguzi huo ni leseni ya udereva, Kitambulisho cha Utaifa na hati ya kusafiria.

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo na Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima akizungumza na TUMBUSI BLOG na kwamba matumizi ya hati hizoyatapunguza biashara ya watu kununua au wizi wa vitambulisho vya kupigia kura na kuongeza uwanda mpana wa mtu kupiga kura. 

"Hati ya kiapo cha mahakama cha kuthibitisha majina yako na taarifa zako haitaruhusiwa kupigia kura katika uchaguzi huu mdogo, kuna hati tatu tu ambazo zitaruhusiwa kutumika,"amesema.


Kailima amesema hati mahakamani haitatambuliwa na kutoruhusiwa kwa namna mbili ikiwemo kutokuwa na mtiririko wa majina ya mpiga kura na kwamba yanatakiwa mtiririko huo ufanane kwa maneno na herufi.

"Huna kitambulisho cha NIDA, leseni ya udereva, hati ya kusafiria umekwenda mahakamani umeapa haitakubalika, Tume kwa mamlaka iliyonayo imesema kwa mujibu wa Sheria mwenye vitambulisho vitatu na hivi vitatumika kwenye uchaguzi mdogo wa Kata 43,"amesema.


Amesema ukifika uchaguzi Mkuu, Tume itatoa maelekezo mengine na kwamba hayo ni maelekezo ya uchaguzi mdogo wa Kata hizo kutokana na matakwa ya sheria na kutokuboreshwa kwa daftari la kudumu la wapiga kura.


"Hii ndiyo tunaanza kupiga kura kwa hati hizo tatu, kutokana na kutokuboresha daftari,ili isipoteze haki ya mtu kupiga kura na tumeona uwanda wa NIDA ulipofika watu wanaweza kuwa na vitambulisho, pia leseni za udereva watu wengi wanazo ikiwemo maeneo ya vijijini madereva wa pikipiki wanazo"amesema.


Amesema fomu za uchaguzi huo imeanza kutolewa leo hadi Oct 26,mwaka huu ambazo zinapatikana kwa Mkurugenzi wa Halmashauri au Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata.


"Mwisho Oct 26 mwaka huu saa kumi jioni, baada ya hapo fomu za wateule zitawekwa sehemu za wazi ili kutoa fursa ya kuwekewa pingamizi ambapo wanaoruhusiwa kufanya hivyo ni Mgombea mwenza wa Udiwani kwenye Kata husika.


"Si kutoka Kata nyingine, Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo na Msajili wa Vyama vya siasa kutokana na sheria za gharama za uchaguzi na kama msimamizi wa uchaguzi akimwekea pingamizi mgombea itabidi aweke rufaa ikishindikana inaamia NEC iwapo kama pande mojawapo ikishindwa kukubaliana na maamuzi ya kamatiya rufaa ya pingamizi itakuwa kesi baada ya uteuzi.


Katika uchaguzi huo wapiga kura zaidi ya 300,000 wanatarajia kupiga kura katika vituo zaidi ya 800 na Kata 43.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...