Skip to main content

LHRC YAPINGA ADHABU YA KIFO


KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeitaka serikali kubadilisha sharia, kuondoa adhabu ya kifo kwa kuweka adhabu mbadala kwenye makosa ya jinai na wafungwa waliopo katika vifungo vya muda mrefu gerezani.


Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na waandishi wa habari juu ya kupinga adhabu ya kifo leo jijini Dar es Salaam.


Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na Mtandao wa Matukio360, amesema kuwa kituo hicho kinaungana na Mtandao wa Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani katika maadhimisho ya 15 siku ya kupinga adhabu ya kifo.


Henga amesema adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili ambayo inakinzana na misingi ya utu na haki za binadamu kama ilivyoainishwa katika mikataba mbalimbali ya kimataifa.


“Adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili isiyo ya staha, inayotweza utu wa binadamu, inafanya serikali ionekane pia kama mhalifu kwa kuua, tuitake serikali ibadilishe sharia na kuondoa adhabu ya kifo na kuweka adhabu mbadala kwenye makosa ya jinai na kwa wafungwa waliopo mfano vifungo vya mrefu,” amesema Henga.


Aidha LHRC kime mpongeza Rais John Magufuli kwa kuweka wazi msimamo wake wa kutounga mkono adhabu ya kifo kwani ni ya kinyama na isiyostahili binadamu yeyote.


Kwa upande mwingine Henga ametoa sababu za kituo hicho kupinga adhabu hiyo. Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na adhabu kuwa ya kibaguzi kwani mara nyingi wanaopatikana na hatia na kupewa adhabu hiyo ni maskini wasioweza kuwa na ushauri wa kisheria na watu wengine.


Nyingine ni vigumu kuthibitisha kuwa inatekelezwa tu kwa watu ambao wametenda na kukutwa na hatia ya kosa hili au wabaya Zaidi, Adhabu hiyo ikitolewa kwa mtu asiye na hatia kimakosa huwezi kuirekebisha kwani mfumo wa utoaji haki huwa pia na uwezekano wa kuwa na mianya ya makosa.


Ameongeza nyingine kuwa ni adhabu kutompa nafasi mtuhumiwa kujirekebisha bali ni ya kulipiza kisasi na wala haimsaidii mtu yeyote hata familia ya muathirika, hakuna ushahidi wowote kuwa adhabu hiyo inazuia watu wengine kutokwenda makosa kama hayo.


Pia amesema sharia hiyo inamianya ya makosa na ni vigumu kuwa na uhakika kuwa haki itatendeka kila wakati. Wapelelezi –ubambikiwaji wa kesi, changamoto za kiupelelezi, waendesha mashtaka, huweza kufanya makosa, majaji kufungwa mikono kulingana na uwakilishi mbele yao na kubanwa na sharia inayowataka kutoa adhabu ya kifo kwenye makosa tajwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...