Skip to main content

MAFAMASIA NA WAFANYABIASHARA WA DAWA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA...,











PICHA ZOTE NA FRIDAY SIMBAYA

Wafamasia na wafanyabiashara wenye maduka binfasi ya dawa za binadamu na mifigo wameombwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za uuzaji dawa.

Hayo yalisemwa jana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Robert Salim katika maadhimisho ya ‘Siku ya Famasi’ yaliyoandaliwa na chama cha wanafanzi wa famasi –Tanzania (TAPSA), tawi la Chuo Kikuu Katoliki cha Ruaha (RUCU) kwa ufadhili wa shirika la Austrian Leprosy Relief Association kwa kushirikiana shirika la Action Medeor.

Maadhimisho hayo ambayo yalienda sambamba na kaulimbiu isemayo, ‘MAPAMBANO DHIDI YA USUGU WA DAWA NI YA KILA MMOJA WETU.’ 

Dkt. Salim alisema kuwa wafamasia na wafanyabiashara wanatakiwa kuuza dawa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu kwa mfano, kuuza dawa za moto kwa prescription na kutunza dawa vizuri.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ina lengo la kuifikisha nchi katika uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda.

Mganga mkuu huyo aliviomba vyuo vyote nchini vya famasi viwaandae vijana kufungua viwanda vya dawa na vifaa tiba kwa vile malighafi nyingi zipo hapa Tanzania.

“Kuna mistu, pamba, gypsum na kadhalika ambazo ni hazina kubwa ya dawa za tiba asili,” alisema Dk. Salim.

Pia, aliwataka wanafunzi wanaosomea masomo ya famasia wa kimaliza masomo yao waanzishe viwanda vidogo vidogo vya dawa, ili kutimiza adhima ya serikali ya awamu ya tano ya sera ya viwanda ambapo kutasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijina.

Naye, Mwenyekiti wa TAPSA-RUCU Ndamo Adam alisema kuwa usugu wa dawa ni janga la kifaifa husuani nchi ambazo zipo katiak ukanda jangwa la sahara kusini.

Alisema kampeni ya kupambana na usugu wa dawa ni jukumu la kimoja kwa vile dawa zote zinazotumika kutibu magonjwa ya kuambukiza huweza kuathiriwa na usugu wa dawa. 

Adam alifafanua kuwa usugu wa dawa ni hali ya dawa kushindwa kuua au kuzuia ukuaji wa vimelea vya magonjwa na vimelea vya magonjwa ndivyo hujenga usugu dhidi ya dawa.

“Dawa zinazotumika mara kwa mara kama vile Ampicilin, Ciprofloxacin, Tetracycilin, Erythromycin, Metronidazole, Amoxicilin, Chloramphenicol na Griseofulvin zinaathiriwa zaidi,” alisema Adam.

Alisema kuwa moja ya usugu wa dawa ni kutotumia ‘dozi’ sahihi ya dwa na kwa muda ulioelekezwa pamoja na kutumiaantibayotiki kutibu magonjwa yasiohitaji antibiotiki.

Kwa upande wake, Mfamasia na mwalimu wa Famasia katika chuo kikuu katoliki cha Ruaha (RUCU) Gasper Baltazary alisema kuwa kampeni dhidi usugu wa dawa iwe endelevu.

Alisema kuwa kuna umuhimu mukubwa wa usimamia ugunduzi sahihi wa magonjwa (kwa vipimo), utoaji dawa kwa dozi sahihi (vipimo), muda sahihi, kuzingatia masharti ya daktari pamoja na kutoa dawa ambazo hazijaisha muda wake wa matumizi.

Baltazary alisema kuwa siku ya famasi ni moja kati ya majukumu ya chama cha TAPSA ambapo lengo ni kuwaleta wanafunzi na wataalamu mbalimbali wa kada ya afya ili kujadili viti ambavyo vinahusu afya.

Alisema kuwa ukosefu wa elimu ndio chanzo kikubwa cha uwepo ya usugu wa dawa, hivyo basi jamii na wafanyabiashara waache kutumia dawa bila kufanya vipimo na kuuza dawa kwa lengo la kupata tu pesa.



Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...