Skip to main content

Miaka 100 ya Skauti: Mkuu wa wilaya Sophia Mjema atoa agizo la uanzishwaji wa klabu za skauti kila...




Mkuu wa wilaya akizindua mapango wa mawasiliano kwa njia ya redio maalumu njia ya upepo na inteneti kwa skauti ‘Jamboree on the Air (JOTA),



Mkuu wa wilaya ya ilala Sophia Mjema Akikagua gwaride maalumu lililoandaliwa kwa ajili yake akiwa ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wilaya ya ilala.


Na Michael Utouh


Mkuu wa wilaya ya Ilala ambae ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi ya wilaya akikagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake na wanafunzi wanaopata mafunzo maalumu ya scout alipofika kwa ajili ya kufunga makambi yao ya mafunzo siku ya leo.





Mkuu wa wilaya akiwahutubia wanafunzi wa scout.










Mmoja wa wakilishi wanafunzi wanaopata mafunzo ya scout wakisoma risala yao mbele ya mgeni rasmi.


Mkuu wa wilaya akikapewa maelekezo juu ya mpango anzilishi wenye lengo la kumkomboa mwana scout na baadhi ya mambo mengi kama vile Elimu nk.



Akitembezwa pamoja na kukagua baadhi ya makambi ambayo wameyaweka wanafunzi hao kwa ajili ya mafunzo yao.




Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amemuagiza afisa elimu wa wilaya ya Ilala kuhakikisha kila shule inafanya uandikishaji wa wanafunzi kwa ajili ya mafunzo ya vikundi vya skauti nakila shule ihakikishe inatoa mwalimu mmoja kwa ajili ya kusimamia vikundi hivyo.



Mjema ameyasema hayo katika kuadhimisha miaka 100 ya skauti tangu kuanzishwa kwake 1917 sambambana kuzindua wiki mawasiliano ya anga kwa njia ya upepo na inteneti kwa skauti ‘Jamboree on the Air (JOTA), Jamboree on the Internet (JOTI)’yaliyofanyika katika shule ya Sekondari Pugu Jijini Dar es Salaam.


“Ikama ya walimu wa skauti ni ndogo natoa agzio kwa afisa elimu kufanya uandikishaji wa skauti wakike na wakiume katika kila shule na kuhakikisha kila shule kunakuwa na mwalimu mmoja ambaye atakuwa anawafundisha skauti hao” Amesema Mkuu wa wilaya

DC Mjema ameeleza kuwa skauti wengi ni vijana wakifundishwa maadili mema Tanzania itakuwa ni yenye umma bora na watu wake watakuwa na uzalendo na Taifa la Tanzania.


“Skauti wengi ni Vijana hivyo ni wajibu wao kutengeneza ulimwengu bila madawa ya kulevya, bila maovu , kutengeneza skauti wazalendo wenye tija na Taifa la Tanzania, pia wanapopata fursa mbalimbali za nje ya nchi wasisite kuitangaza Tanzania kwa kueleza mema ya Tanzania ikiwemo Amani, Muungano na Rasilimali zilizopo” Amesema. 

Pia DC Mjema ametoa wito kwa watoto na skauti wote pindi wanapoona matukio ya kidhalilishaji au kufanyiwa watoe taarifa kwa mamlaka kwa mamlaka husika kwani serikali ipo kwa ajili yao na itawalinda. 

“Wenyeviti wa Serikali za Mtaa, Wakuu wa Wilaya, Mawaziri, mpaka ngazi ya juu ya Rais chini ya Rais John Pombe Magufuli tutahakikisha tunazilinda na kuzitetea haki za mtoto hivyo wasiogope kutoa taarifa za unyanyasaji kijinsia hata kama wakitishiwa maisha yao” Amesema. 

Katika hatua nyingine DC Mjema amehaidi kushughulikia moja ya changamoto iliyotolewa na wawakilishi wa uongozi wa skauti kuhusiana na eneo la kambi na eneo kwa ajili ya kilimo ambapo amewahakikishia uwepo wa maeneo hayo kwa kumuagiza Mkurugenzi kuwapa kipaumbele pale watakapo ainisha maeneo kwa ajili ya viwanda vidogo kwani kufanya hivyo ni kuwakwamua kiuchumi. 

“Namuagiza Mkurugenzi kushughulikia suala la eneo la kilimo, pia ni vyema mkaja ofisini kwangu siku ya Alhamisi ili niwakutanishe na Afisa Maendeleo kwa ajili ya kujadili na kufikia malengo yenye tija kwa skauti na taifa kwa ujumla” Amesema. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...