Skip to main content

WADAU SEKTA YA AFYA WATAKA SHERIA YA CHF 2001 IBORESHWE




WADAU wa sekta ya afya wameomba Sheria ya mfuko wa afya jamii (CHF) ya mwaka 2001 kufanyiwa mapitio ili ionesho fedha ya fidia kwa huduma iliyotolewa kwa makundi yenye msamaha itatoka wapi na taratibu za namna fidia hizo zitakavyotolewa ili ziongeze fedha kwa ajili ya manunuzi ya dawa.

Wadau hao walisema hayo jana katika kikao cha kujadili changamoto katika utoaji wa huduma za afya wilayani Iringa kilichoandaliwa shirika lisilo la kiserikali la TACOSODE kupitia mradi uwajibikaji jamii katika sekta ya afya (CEGO).

Kikao hicho kilijumuisha waganga wa zahanati na vituo vya afya, madiwani,watendaji wa kata, afisa mipango wa wilaya, afisa maendeleo ya jamii, mganga mkuu wa wilaya na mratibu wa CHF.

Walisema kuwa Serikali itenge na kupeleka pesa za fidia kwa huduma za afya zinazotolewa kwa makundi maalum ambayo hupata huduma za afya kutoka kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati.

Kwa vile makundi hayo yamekuwa yatumia fedha nyingi za wananchama wa CHF.

Makundi yenye msamaha hawachangii huduma za afya na kunafanya wanachama au wanachaniaji wa CHF kubebeshwa mzigo kwa vile vituo havitoi fidia.

Sheria ya CHF ya mwaka 2001 kufungu cha 10(1) inazipa kamati za afya za kata mamlaka ya kutoa misamaha kwa makundi maalumu kama vile wajawazito, wazee, walemavu na watoto chini ya miaka mitano.

Kifungu 10 (2) kinazipa kamati hizo kutoa fidia kwa huduma za afya zilizotolewa kwa makundi hayo, lakini sheria hiyo haielezi mahali ambapo kamati hizo zitoa fedha za kufidia huduma zilizotolewa.

Walisema kuwa huko ni kuacha mzigo huo migogoni mwa wanachangiaji wa CHF na kuwakatisha tamaa ya kuendelea kuchangia mfuko na hivyo kuendeleza wimbi la uhaba wa dawa, vitendanishi na vifaa tiba.

Kwa upande wake, Mratibu wa mfuko wa afya jamii (CHF) halmashauri ya wilaya ya Iringa Dora Mlomo alisema kuwa kuna uchangiaji hafifu wa wananchi katika mfuko huo kupelekea kushindwa kutoa huduma za afya.

Mlomo alitoa rai kwa wananchii kujiunga na mfuko huo ilikuweza kuboreshaji wa utoaji huduma za afya kwani kwa mwaka kaya inatakiwa kichangia shilingi elfu kumi (10).

Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kujiunga kwa wengi ili fedha zinapatikana kwa wengi ilikweza kuwahudumia hata makundi yenye msamaha.

Naye, diwani wa kata ya mlowa, Charles Nyagawa alisema kuwa wanasiasa ni chanzo cha kuzoretesha maendeleo katika maeneo mbalimbali nchi. 

Alisema kuwa kuna baadhi ya wanasiasa wanaamasisha wananchi wasichagie maendeleo kwa mfano ujenzi wa zahanti au shule na kufanya miradi kushindwa kutekelezeka.

Nyangawa alisema kuwa suala la maendeleo lisichanganywe na siasa isipokuwa wanasiasa waungane kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Alisema kuwa wanasiasa kutoka chama tawala (CCM) na wale wa upande wa pili waunge mkono juhudi za serikali katika kutekeleza sera za chama hicho.

Mratibu kutoka TACOSODE Abrahamu Kimuli Mkutano ulikuwa na lengo la kubadilishana uzoefu juu ya masuala yaliyotolewa na TACOSODE wakati wa CEGO katika utekelezaji wa mradi wa afya katika halmashauri za wilaya za Iringa na Kongwa.



Kwa USAID mkutano ulikuwa uliangalia fidia ya CHF kwa makundi maalum yaani fidia, usimamizi na utawala kwa "Sheria ya CHF ya 2001" na kupendekeza njia mbadala.


Alisema kuwa Wizara ya Afya inatakiwa kupitia upya taratibu za fidia, usimamizi na utawala wa CHF kama ilivyoelezwa kwa sheria CHF mwaka 2001 ili kupunguza mzigo kwa wanachama wa CHF.

Naye mkurugenzi mtendaji wa TACOSODE Theofrida Kapinga serikali itenge bajeti angalau ifike kiwango kinachopendekezwa katika Azimio la Abuja ambacho ni asilimia 15 ya bajeti yote ya serikali.

Alisema kuwa serikali inatakiwa kusimamia mapato ya ndani kwa vile wahisani wako mbioni kupunguza uchangiaji wa fedha katika sekta ya afya ili kuweza kujitengemea.

Kapinga alisema serikali ipeleke fedha zote zilizoidhinishwa na kwa wakati ili kuwezesha miradi na huduma za afya kufanyika kama ilivyopangwa ili kuepusha kutoa huduma chini ya kiwango vilivyokushudiwa.



Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...