Skip to main content

WANA GDSS WAFANYA UCHAMBUZI NA KUANGALIA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA BAJETI YA TAIFA


Washiriki wa semina za jinsia na maendeleo (GDSS) wamekutana jumaatano hii lengo likiwa ni kujadili ushirikishwaji wa moja kwa moja wa wananchi katika upangaji wa bajeti kuu ya taifa.

Mlaghbishi wa semina ya GDSS wiki hii Bw. Hancy Orote akitoa ufafanuzi juu ya jambo fulani katika semina iliyofanyika mapema wiki hii makao makuu ya TGNP Mtandao Mabibo Dar es salaam.


Akiongoza semina hiyo mwanaharakati kutoka GDSS Bw. Ance Obote alisema dhumuni la kukutana mahali hapo ni wanaharakati kubadilishana uwezo kuhusu ufahamu, ushiriki na jinsi gani wanatoa elimu hiyo kwa wananchi kuhakikisha wanaitumia haki yao ya msingi ya kushiriki katika bajeti.


Muwezeshaji huyo amesema kuwa wananchi huusika sehemu kuu mbili ambazo ni kwenye kupanga vipaumbele na ufuatiliaji(utekelezaji) lakini wananchi hawapewi nafasi ya kupanga vipaumbele na kinachofanyika ni diwani anakutana na mtendaji wa kata na kupanga kipi kianze kama kipaumbele na kipi kiwe cha mwisho.
Mshiriki wa semina za GDSS Bw. Geofrey Chambua akitoa mchango wake katika semina iliyofanyika mapema wiki hii Mabibo jijini Dar es salaam.


Na jambo lingine ni kwamba kwa maeneo ya mijini hakunaga vikao vinavyokaliwa na kujadili maendeleo ya mtaa ama kata hivyo mambo yanaendeshwa kienyeji na mambo mengi yanayofanywa yanakuwa ni akili za viongozi na siyo mawazo ya wananchi hali inayoweka ugumu katika utekelezaji wa mambo mengi kama hili la kuweka vipaumbele.


Aidha wanaharakati wameamua kuweka utaratibu wa kujipima kwa kuangalia harakati zao zinafika umbali gani na katika hili wameamua kupeleka ushawishi katika kata walau tatu na kuja kuangalia ushawishi wao wa kubadilisha dhana hii ya viongozi kupanga vipaumbele wenyewe bila kushirikisha wananchi inaweza kuisha?.
Bw. Msafiri Shabani akitoa maoni yake ya nini kifanyike ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya moja kwa moja ya kushiriki katika kupanga vipaumbele katika bajeti ya Taifa.


Lakini pia kupitia semina hiyo wanaharakati wameweka mipango mbalimbali ya kufuatilia jambo hilo na kugawana majukumu mpaka ifikapo tarehe 29 novemba kila kundi lililochaguliwa kufuatilia katika kata husika liwe limeleta mrejesho wa kilichopatikana na mgawanyo wenyewe ulikuwa kama ifuatavyo.


Washiriki wa semina za GDSS wamepewa majukumu ya kufuatilia katika serikali zao za mitaa kwa kuwahoji viongozi wa mitaa yao na kuleta mrejesho kwanini wananchi hawapati nafasi ya kushiriki katika kupanga vipaumbele na matokeo yake wanahusishwa katika hatua za mwisho ambazo ni utekelezaji.
Baadhi ya washiriki wa semina za GDSS walioudhulia mapema wiki hii.


Lakini vituo vya taarifa na maarifa wao wameombwa kufuatilia serikali kuu hii ikiwa ni katika wizara mbalimbali zinazohusika na hili ili kuweza kukusanya majibu ya serikali za mitaa pamoja na wizara kuweza kuwa na jibu moja lililokamilika kuhusu swala hilo.


Na jambo lingine ni kuabadilisha mtindo wa kuingia katika sekta hizi kwani wengi uenda kwa njia ya kujiita wanaharakati jambo ambalo linawafanya watu hawa kuwaona wao ni wapinzani na kuweka chuki miaongoni mwao, na pia imeelezwa sio vizuri kwenda mtu mmoja mmoja na wanatakiwa kuunda makundi madogo madogo yatakayowafanya waonekane ni wananchi kweli wanaohitaji taarifa za kata au mtaa wao.
Baadhi ya wanaharakati wakifuatilia kwa umakini semina iliyoendeshwa na Hancy Orote mapema wiki hii Mabibo Dar es salaam.


Aidha wanaharakati wameshauriwa kufanya kazi kwa moyo wa kijitolea na kuleta mabadiliko katika jamii yao na siyo kufanya ili waonekane na TGNP au kwa ajiri ya kuleta ripoti kwa mtu Fulani bali wafanye kwa manufaa yao na jamii iliyowazunguka. 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...