Skip to main content

WAZAZI WA KWAMISHA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI


Baadhi ya wazazi wakifuatlia kikao cha wazazi katika Shule ya msingi Muungano manispaa ya IRINGA, mkoani IRINGA leo. (Picha na Friday Simbaya)

IRINGA: SHULE ya msingi Munnugano katika manispaa ya Iringa, mkoani Iringa imesitisha mpango wakutoa uji kwa wanafunzi kwa muda kutokana na wazazi kusuasua kutoa michango.

Hayo yalielezwa na mwalimu mkuu wa shule ya msingi muungano Richards Nchimbi wakati wa kikao cha wazazi kilicholenga kutamubulisha kamati mpya ya mpango jamii wa uhamasishaji na utekelezaji elimu (MJUUE) Ushirikiano wa Wazazi na Waalimu (UWAWA) jana kupitia program ya USAID Tusome Pamoja.

Alisema kuwa kutokana na wazazi kutoona umuhimu wa watoto wao kupata uji mwalimu mkuu kwa kushirikiana na kamati ya shule hiyo wamesitisha mpango wa chakula shuleni hadi hapo baadaye.

Nchimbi alisema kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 700 lakini ni watoto kumi (10) tu kwa sasa ndio wanaokunywa uji shuleni na kupelekea kushindwa kulipa gharama ya mpishi ya shilingi 60 kwa mwezi.

“Tulikuwa na utaratibu wa kutoa uji kwa wanafunzi wote ambapo kila mzazi anatakiwa kuchangia shilingi 2000 kwa mwezi lakini wazazi wengine wameshindwa kutoa michango wa uji kwa wanafunzi,” alisema Nchimbi.

Naye mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi muungano saidi lawa alisema shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu mibovu ya vyoo vya wanafunzi na walimu, uchakavu wa vyumba vya madarasa na kutokuwa na viwanja vya michezo.

Alisema kuwa kupitia mpango jamii wa uhamasishaji na utekelezaji elimu (MJUUE) wamepanga kukalabati vyoo vya wanafunzi ambapo gharama za ukarabati zitagharimu zaidi ya shilingi milioni mbili (2m/-) ambapo kila mzazi mwenye mtoto anatakiwa kuchangia shilingi elfu tano. (5000/-).

Lawa alisema kuwa ili kuboresha mazingira ya ufundishaji na kujisomea serikali kwa kushirikiana na jamii wanabudi kutoa michango ya mali na hali ili kuboresho ufaulu kwa wanafunzi.

Kwa upande wao Washiriki wa Mahusiano ya Jamii (CEF) mradi wa USAID Tusome Pamoja, Winston Ngowo na Sara Ndoto walisema kuwa mradi wa elimu wa miaka mitano unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Watu wa Marekani (USAID).

Walisema kuwa Mradi huu unalenga kusaidia kuboresha stadi za ufundishaji na kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) katika shule za awali na madarasa ya chini ya shule za msingi (1-4), katika mikoa minne ya Tanzania bara (Iringa, Morogoro, Mtwara na Ruvuma) pamoja na shule zote za serikali Zanzibar. 

Pamoja na kutoa mafunzo kwa walimu , vitabu kwa wanafunzi, malengo zaidi ya mradi wa USAID Tusome Pamoja ni kuimarisha ushiriki wa wazazi na jamii kwenye elimu kupitia kamati za shule, Ushirikiano wa Wazazi na Waalimu ( UWAWA) na jamii yote kwa ujumla.

Hivi Karibuni,USAID Tusome Pamoja ikishirikiana na serikali katika mikoa huu, iliendesha mafunzo ya mpango jamii wa uhamasishaji na utekelezaji elimu (MJUUE) wenye lengo la kuhamasisha jamii katika kubaini changamoto katika sekta ya elimu zinazo athiri ubora wa elimu na ufaulu; Kubaini rasilimali na utatuzi wa changamoto hizo.

Pia mafunzo haya yalilenga (kusaidia jamii ishiriki katika kuandaa mipango ya elimu kwa ajili ya watoto wao hivyo kuimarisha ushiriki wa jamii katika kuboresha utoaji wa elimu.

Kupitia mpango huo USAID Tusome Pamoja unaotekelezwa na shirika la Care International kwa shirikia na RTI International, ilitoa mafunzo ya siku tatu kwa Wawezeshaji Jamii Elimu 968 kutoka shule 481 za msingi za serikali mkoani Iringa.

Walisema kuwa pamoja na mambo mengine wameweza kusaidia kuongoza uandaaji wa dira na mipango kazi ya muda mfupi ya shule zao za msingi.

Na mipango hiyo kuridhiwa na jamii, Wahamasishaji hawa baada ya kupata mafunzo pia wanafanya kazi ya kujitolea ya kuhamasishaji jamii kushiriki katika shughuli zote zinazohusu elimu katika shule zao. Na Friday Simbaya, Iringa

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...