Skip to main content

DC KASESELA AONGOZA OPRESHENI KWA WAFANYABIASHARA WASIOTUMIA EFD


Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongozana na meneja wa TRA na maafisa wake mkoa wa Iringa akikagua matumizi ya mashine za kutolea risiti.



NA DENIS MLOWE, IRINGA

MKUU wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ameongoza opareshEni kubwa ya kuwasaka wafanyabiashara wasiotumia risiti za mashine (EFD) katika madukani mbalimbali manispaa ya Iringa.

Katika oparesheni hiyo iliyofanywa katika eneo la Miyomboni ilihusisha wafanyabiashara wa maduka mbalimbali ambapo wengi wao wamekutwa na makosa ya kutotumia mashine hizo katika uuzaji wa bidhaa au wakati mwingine kuandika bei ya chini kuliko bidhaa.

Akizungumza mara baada ya oparesheni hiyo, Kasesela amewataka wafabiashara kutumia mashine za kutolea risiti kila wanapouza bidhaa zao na jamii kudai risiti kila wakati baada ya kubaini asilimia kubwa hawatumii EFD mara kwa mara..

Alisema kuwa serikali inawategemea sana wafanyabiashara kulipa kodi lakini serikali haitasita kuwachukulia hatua wafanyabiashara wasiolipa kodi zao kwani wanarudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Kasesela alisema kuwa changamoto ambazo wamezibaini kwa wafanyabiashara hao ni kutotumia mashine mara kwa mara na kuwataka TRA kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa wafanyabiasharac wote na wakibainika wasiotii sheria wafungiwe maduka yao.

Katika oparesheni hiyo jumla ya maduka mawili yalifungiwa ambapo Kasesela aliwapatia siku tatu kuhakikisha wanamaliza kulipa kodi, na kubadilisha majina ya umiliki wa biashara kwa mamlaka mapato Tanzania.

Kwa upande wake Meneja mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Iringa, Lampson Tulianje amesema kuwa wafanyabiashara wa wengi wana mwitikio mdogo wa kutoa risiti za EFD baada ya kufanya ukaguzi katika maeneo mbalimbali na kubaini hilo.

Tulianje alisema kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa zao pasipo kuwapatia risiti za mashine za Kielektroniki (Efd) wateja wao mara kwa mara hali inayokosesha TRA mapato hivyo pindi wakibainika wanafikishwa katika vyombo vya sheria na kuchukua mali zao hadi wamalizapo.

Alisema kuwa kampeni hiyo imeendelea kufanyika katika maduka yote mkoani hapa kwa kushtukiza hali ambayo wanakutana nayo ni wafanyabiashara hao kutoa risiti kwa wateja wachache tofauti na wanavyowahudumia wateja wengi kwa siku.

Alisema kuwa kutona na hali hiyo TRA mkoa wa Iringa itaendelea kufanya zoezi hilo kuhakikisha wafanya biashara wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za biashara katika mauzo ya bidhaa zao kwa kutoa risiti kwa kila mteja wanayemhudumia.

Tulianje alisema kuwa kila bidhaa inayouzwa inapaswa kutolewa risiti, zikiwamo bia hivyo, maafisa wa TRA watafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha wafanyabiashara wote ambao wanahitajika kutumia mashine hizo wanatumia ili kuingizia mapato serikali.

"Lengo la TRA sio kuwafungia biashara hawa wafanyabiashara lakini endapo watashindwa kufata sheria hatua stahiki zitachukuliwa bila hofu yoyote na hatupendi kuwapiga faini lakini italazimika kufanya hivyo, kwani tunasimamia sheria na imeonekana idadi kubwa ya wafanyabiashara mkoani hapa hawatumii mashine za EFD kama ambavyo inatakiwa,"alisema.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...