Skip to main content

MAAZIMISHO YA AROBAINI YA IMAM HUSSEIN : SHEIKH JALALA ATAKA WAISLAMU KUENZI MAFUNDISHO YAKE




Ikiwa bado siku moja kukamilika kwa siku ya arobaini tokea kujitoa muhanga kwake Imam Hussein ambaye pia ni Mjukuu wa Bwana Mtume Muhammad (S.AW), Watanzania wametakiwa kuenzi mafundisho yake kwani enzi za uhai wake Imam alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa utukufu wa mwadamu, heshima yake unaenziwa kwa kiasi kikubwa na pia hakuna ubaguzi wa aina yoyote unao endekezwa.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake, Kiongozi Mkuu wa Waislam Dhehebu la Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Hemed Jalala amesema Waislamu takribani Milioni 30 watakwenda katika kaburi la Mjukuu huyo wa mtume kuazimisha siku hiyo huku wakikumbuka mafunzo yake matakatifu ya kumtukuza Mwanadamu na kupinga kabisa aina yeyote ya ukandamizaji na unyanyapaa kushamiri miongoni mwa Wanadamu.

“Imam Hussein alikuwa ni mtu aliyependa kuenzi utakatifu, utukufu na kuheshimu utu wa Mwanadamu…darsa zake zote ukizisoma utaona alikuwa akisisitiza kuhusu watu kushirikiana, hakupenda kabisa watu kunyanyapaliana, kuwepo kwa matabaka… nadhani hata sasa dunia inahitaji kuwa na mafundisho kama hayo” Alisema Sheikh Jalala.

Inaelezwa kuwa Imam Hussein (a.s), ambaye ni Mjukuu wa Bwana Mtume Muhammad (s.a.w.w), alijitoa Muhanga siku ya Ashura, maisha yake na familia yake na Masahaba zake kwa ajili ya kupigania Haki na Ubinadamu uliokuwa umekanyagwa na Mtawala anayedaiwa kuwa dhalimu Bw. Yazid Ibn Muawiyyah.


KWA UFUPI 
Imam HUSSEIN (a.s). Kwa ufupi, Imam Hussein ni kiongozi aliyeonesha dira ya namna ya kupambana na DHULMA ulimwenguni kama Mahatma Gandhi (Baba wa Taifa la India) na Rabindranath Tagore (Indian Nobel Prize in Literature 1913), Thomas Carlyle (Scottish historian and essayist) , Charles Dickens (English novelist) Edward G. Brown (Professor at the University of Cambridge walivyomulezea Imam Hussein katika maandishi mbalimbali wakihusianisha mafanikio ya harakati nyingi za kudai haki na Imam Hussein (A.S).

Kwa huzuni kabisa, tunatoa mkono wa pole kwa Mtume (s.a.w.w) na familia yake (Ahlulbayt), pia kwa waislam wote ulimwenguni na wapenda haki pasina kujali imani zao.
Imam Hussein ni kielelezo cha utu, uadilifu, na amani. Pia ni ishara ya ukombozi wa viumbe na ni kielelezo cha kupinga dhulma ulimwenguni.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...