Skip to main content

MBOWE AWATAKA KITWIRU KUFUNGUA VYUMA KWA KUINYIMA KURA CCM























MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amewataka wapiga kura wa kata ya Kitwiru, Mjini Iringa kupeleka ujumbe wa hali ngumu ya maisha kwa Rais Dk John Magufuli kwa kumchagua mgombea wa chama chake kuwa diwani wa kata hiyo.


“Wakati wananchi wakilalamika vyuma vimekaza, watu hawana hela mifukoni, manunuzi yanapungua na baadhi ya biashara ndogo, za kati na za wawezekazaji wakubwa zikifungwa, kuna baadhi ya madiwani wa upinzani wananuliwa kwa kati ya Sh Milioni 2 na Milioni 5 halafu hela za kodi zinazolipwa na watanzania masikini zinatumika kuitisha chaguzi ndogo kwa gharama kubwa,” alisema.


Mbowe alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekuwa ikitumia hadi Sh Milioni 200 kugharamia uchaguzi wa kata moja ambayo diwani aliyekuwepo ananunuliwa kwa Sh Milioni 5.


Akizungumzia hali ya maisha ya mtanzania kwasasa Mbowe aliwauliza mamia ya wanachi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni uliomnadi mgombea wao udiwani wa kata hiyo Bahati Chengula tofauti ya kipato na hali ya maisha wanavyoina sasa na wakati wa utawala wa Jakaya Kikwete; wote walinyosha vidole wakiashiria wakati wa Kikwete hali ya maisha ilikuwa na nafuu.


Katika mkutano huo Mbowe alizungumzia pia masuala mbalimbali ikiwemo deni la Taifa akisema kwa sasa kila mtanzania wakiwemo watoto wachanga anadaiwa wastani wa Sh Milioni 1.2.


Akazungumzia pia hali ya kisiasa na jinsi wanasiasa wanavyozuiwa kufanya mikutano, kusitishwa taarifa za moja kwa moja za bunge, shambulio dhidi ya Mbunge Tundu Lissu, na jinsi chama hicho kilivyompokea kwa mikono miwili, Lazaro Nyalandu.


Akiomba kura, mgombea wa udiwani wa kata hiyo aliwaomba wapiga kura wa kata hiyo wamchague kuwa diwani wao ili akaungane na madiwani wanaounda halmashauri ya manispaa ya Iringa kupitia chama chake hicho kushughulikia changamoto mbalimbali za kimaendeleo.


"Nayafahamu matatizo ya kata hii katika sekta zote ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu ya barabara, maji, maeneo ya biashara na mengine mengi, Nipeni kura nikawatumikie," alisema.


Naye Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema anaingiza miguu yote katika kampeni za kata hiyo kuanzia kesho.


"Vikao vya bunge vinamalizika kesho, siendi tena bungeni, siku kumi zote zilizobaki nitabanana katika kata hii hadi kieleweke," alisema. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...